Wednesday, February 15, 2017

KIKAO CHA KUJADILI KANUNI ZA LOCAL COTENT

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akimsikiliza mmoja wa washiriki katika kikao cha kuandaa Kanuni za Local Content. Wengine katika picha ni wenyeviti wa Bodi za Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Wakuu wa Mashirika pamoja na Viongozi Waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake na wawakilishi wa kampuni za Wachimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia Nchini.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akisikiliza mada kuhusu Local Content iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Mgamlagosi (hayupo pichani). Wengine ni washiriki walio hudhuria kikao hicho mjini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Ntalikwa (wa pili kulia) akiendesha kikao cha kujadili Kanuni za Local Content kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya BG, Marc Hartog (wa kwanza Kulia) Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Profesa Sufiani Bukurura (wa tatu kulia), Kaimu Kamishna wa Nishati na masuala ya Petroli, Mhandisi Innocent Luoga (wa nne kulia), Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Modestus Lumato (wa tano kulia) pamoja na Viongozi Waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Madini.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akisikiliza mada kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Mgamlagosi (hayupo pichani). Kutoka kushoto, Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Profesa Sufiani Bukurura, wa pili ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Ntalikwa na wa tatu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya BG, Marc Hartog wakiwa katika kikao hicho mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Mgamlagosi (aliyesimama) akitoa ufafanuzi kuhusu mada zilizotolewa kwenye kikao cha kujadili Kanuni za Local Content kwenye Ukumbi wa Wizara ya Nishati na Madini mjini Dodoma. Wanaofatilia ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa kwanza kulia) pamoja na Wenyeviti wa Bodi za Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Wakuu wa Mashirika na Viongozi Waandamizi kutoka Wizarani.
Washiriki wa kikao cha Local Content wakifatilia kikao kilicho jadili Kanuni za Local Content mjini Dodoma.


………….


Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Wachimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia nchini, Wenyeviti wa Bodi za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, Wakuu wa Mashirika pamoja na Viongozi Waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake ili kujadili Kanuni za Local Content kikao hicho kilifanyika tarehe 11-12 mjini Dodoma.

No comments: