Monday, February 6, 2017

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT. JUMA MALEWA APOKELEWA KWA KISHINDO MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akipokelewa na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza alipowasili Makao Makuu ya Jeshi hilo baada ya kuapishwa rasmi kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 6, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akipokea salaam ya heshima toka katika Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari(hawapo pichani) kwa ajili yake kwa heshima.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza kwa ajili yake kwa heshima kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga(kulia) akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa kabla ya kuongea na Maafisa na askari wa Jeshi hilo Makao Makuu ya Magereza mara baada ya kutoka kuapishwa kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza.
Baadhi ya Askari wa Jeshi la Magereza wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa mara baada ya kutoka kuapishwa kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 6, 2017.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa mara baada ya kutoka kuapishwa kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 6, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiongea na Maafisa, askari na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza baada ya kutoka kuapishwa kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 6, 2017.
Sehemu ya familia ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa waliohudhuria kuapishwa kwake leo Ikulu, Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja(katikati) ni Mke wa Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Bi. Fatuma Malewa(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiwasili Makao Makuu ya Jeshi la Magereza mara baada ya kuapishwa rasmi kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 6, 2017.

No comments: