Saturday, February 18, 2017

DC SHINYANGA AONGOZA WANANCHI KUFANYA MAZOEZI

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro leo Jumamosi Februari 18,2017 amewaongoza wakazi wa Shinyanga kufanya mazoezi katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga. 

Mazoezi hayo yaliyoanza saa 12 asubuhi na kumalizika saa 2 asubuhi yamehudhuriwa pia na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini,Stephen Masele na Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro. 

Akizungumza wakati wa mazoezi hayo Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amesema wakazi wa Shinyanga wataendelea kufanya mazoezi kila siku Jumamosi ili kumuunga mkono Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan .
“Wiki iliyopita mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack alizindua mazoezi kimkoa,tumekubalina tuwe tunafanya mazoezi kila wiki siku ya Jumamosi ili kudhibiti Magonjwa yasiyo ya kuambukiza,nawakumbusha kuwa mazoezi ni afya hivyo wananchi naombeni muendelee kujitokeza kufanya mazoezi”,alisema Matiro. 

Hivi karibuni Makamu wa rais Samia Suluhu aliagiza amewaagiza viongozi wa mikoa na wilaya zote kuweka utaratibu wa kufanya mazoezi angalau kwa mwezi mara Moja.

Alisema kila Jumamosi ya pili ya mwezi itakuwa siku ya mazoezi ambapo aliwaasa wananchi kufanya mazoezi na kuanzisha na kujiunga na vikundi vya mazoezi na serikali itatimiza wajibu wake wa kuweka mazingira mazuri ya kufanyia mazoezi kote nchini.

Mwandishi wetu Kadama Malunde ametuletea picha 33 wakati wa mazoez hayo..Tazama hapa chini
Mratibu wa Mazoezi hayo,Diwani wa kata ya Kambarage Hassan Mwendapole akimkaribisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ili azungumze na washiriki wa mazoezi hayo katika viwanja vya Shycom Mjini Shinyanga
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa mazoezi leo katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na washiriki wa mazoezi hayo
Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akitoa neno kwa washiriki wa mazoezi hayo ambapo alisema mazoezi ni afya na yanajenga upendo na kufahamiana kwa washiriki wa mazoezi
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Stephen Masele akizungumza na washiriki wa mazoezi hayo ambapo aliwahamasisha wananchi kuendelea kujitokeza kufanya mazoezi 
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Stephen Masele akizungumza uwanjani
TAZAMA PICHA ZAIDI WAKATI WA MAZOEZI

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akifanya mazoezi
Mazoezi yanaendelea
Wananchi wakifanya mazoezi
Mazoezi yanaendelea
Mbunge wa jimbo la Shinyanga Stephen Masele(wa pili kulia) akifanya mazoezi
Mazoezi yanaendelea
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro(wa kwanza kulia) akifanya mazoezi
Mazoezi yanaendelea
Washiriki wa mazoezi wakisalimiana baada ya mazoezi
Picha ya pamoja ,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro na baadhi ya washiriki wa mazoezi hayo
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

No comments: