Friday, February 10, 2017

DC ARUMERU ALEXZENDER MNYETI ATOA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU MZEE KAYOMBO

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha Mhe Alexzender Mnyeti akisaini kitabu cha maombolezo kijijini Misasi
 Dc Mnyeti, MD Kayombo na familia nzima ya Mzee Kayombo walipotembelea kaburi la Mzee Kayombo
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Alexzender Mnyeti (Kushoto), na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo wakiwa katika mazungumzo
 Dc Mnyeti akitoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu Mzee Kayombo
 Wakati wa sala kwenye kaburi la Marehemu Mzee Kayombo
 Maombi ni muhimu katika kila jambo

Mazungumzo na Ndegu, jamaa na rafiki

Na Mathias Canal, Mwanza

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha Mhe Alexzender Pastory Mnyeti amezuru kijiji cha Misasi, Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza kutoa pole kwa familia ya Marehemu Mzee Kayombo aliyefariki Dunia siku ya saa mbili usiku katika Hospitali ya Rufaa Bugando, Mkoani Mwanza.

Mhe Mnyeti ametoa salamu za pole kwa wakazi wa Kijiji cha Misasi kwa kumpoteza mshauri katika kijiji hicho ambaye amekuwa nguzo kwa maendeleo ya kijiji sawia na utaratibu wake wa kuhamasisha wananchi kupanda miti ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Mnyeti ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Misungwi kabla ya uteuzi wake kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ameeleza jinsi alivyomfahamu Mzee Kayombo katika kuhakikisha jamii inasonga mbele katika maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.

Mnyeti alisema kuwa Mkoa wa Mwanza umepoteza mtu muhimu ambaye pia atakumbukwa kwa kazi njema alizozifanya wakati wa uhai wake.

Dc Mnyeti ametoa pole kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndugu John Lipesi Kayombo kwa kuondokewa na Mzee wake ambaye ni Mlezi wake tangu akiwa mdogo sambamba na kuisihi familia ya Marehemu Mzee Kayombo kuendeleza mshikamano na kupendana.

Marehemu Mzee Kayombo atakumbukwa kwa mambo mbalimbali aliyoyafanya wakati wa uhai wake pindi alipokuwa kazini ikiwa ni pamoja na kupanda miti katika shule zote alizofundisha, Ujenzi wa shule wakati huo, pia atakumbukwa kwa kuhamasisha ujenzi wa Zahanati ya Misasi.

Marehemu Mzee Antony Raphael Kayombo alifariki saa mbili usiku, siku ya Jumamosi ambapo hadi mauti inamkuta alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kibofu cha mkojo ambao ulianza ghafla tarehe 29/1/2017 na kupelekwa katika hospitali ya Misasi, Baadae hospitaliti ya Sekou Ture na mwishowe Hospitali ya Bugando ambapo alifanyiwa upasuaji ambapo hata hivyo hali yake iliendelea kudhoofika mpaka mauti ilipomkuta.

INNALILAH WAINNAH ILAIHI RAJIUN

No comments: