Monday, January 2, 2017

WAKAZI WA KASULU WAMWOBA RAIS DKT MAGUFULI KUTATUA MGOGORO MIGOGORO YA MIPAKA KATI YA WANANCHI NA HIFADHI YA MISITU YA KAGERANKANDA

Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

CHAMA Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kasulu Kimemuomba Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Magufuli kuitimiza ahadi yake ya kuwasaidia Wananchi wa Wilaya ya Kasulu ya Kutatua Migogoro ya Mipaka inayo endelea baina ya Wananchi na eneo la hifadhi ya Misitu ya kagerankanda kama alivyo wahahidi Wananchi hao Wakati wa Kampeni kutatua kero hiyo endapo watakichagua Chama hicho.

Akizungumza na gazeti hili katibu mwenezi wa Wilaya ya Kasulu Masoud Kitowe alisema wakati wa kampeni Rais aliwaomba Wananchi hao wakichague Chama cha mapinduzi na kuwaahidi endapo watakichagua chama hicho atahakikisha anatatua mgogoro huo na kuongeza mipaka Kwa Wananchi hao waweze kulima,na Wananchi walikichagua chama hicho mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa.

Alisema CCM Wilaya ya Kasulu wanapata shida kuwajibu Wananchi dhidi ya mgoholo unaoendelea katika poli la Kagerankanda Wananchi wanao kutwa Wakilima katika poli hilo wanapigwa na kunyanganywa vifaa vyao kwa madai kuwa hawaruhusiwi kulima katika poli hilo ilihali maeneo ya kulimia katika Wilaya hiyo ni Machache na Wananchi wengi wanategemea kulima Mahindi katika poli hilo.

Kitowe alisema mpaka sasa Dawa zimeshafika katika Wilaya ya Kasulu iliwatu wa TFS waliopewa Dhamana ya kulinda msitu huo wamejipanga kumwagia Tindikari mahindi na Maharage yaliyo pandwa katika poli hilo hali inayoweza kupelekea Wilaya ya Kasulu na wilaya zingine za Mkoa wa Kigoma kukabiliwa na Njaa kwakuwa mazao yanayo limwa katika Msitu huo yanahudumia zaidi ya Wilaya nne za Mkoa wa Kigoma.

Hata hivyo alisema endapo Mazao hayo yataunguzwa na Wananchi wakakosa haki yao na jasho lao likapotea jambo hili sio zuri mazao hayo yanapo vunwa Serikali inapata mapato lakini kila msimu wa mavuno halmashauri wanatoza kila gunia shilingi1000 na wanakusanya mapato Wananchi wengi wanasomesha watoto wao kupitia kilomo wanacho fanya katika poli hilo endapo jambo hilo likifanyika wananchi wengi wataumizwa na kitendo hicho.

" nimuombe Muheshimiwa Rais yeye kama Mwenyekiti wetu wa Chama kilichopo madarakani atusaidie juu ya suala hili ilituweze kulitatua Wananchi wetu wanateseka sana juu ya Mgogoro huuu ,naikumbukwe Rais wetu aliwaahidi Wananchi katika Uwanja Wa umoja Wilayani Kasulu kuwa jambo la kwanza kulitatua itakuwa ni Mgogoro wa Msitu wa Kagerankanda uliodumu kwa kipindi cha Muda mrefu na Suala hili hata kwenye ilani yetu ya Chama lipo",alisema Kitowe.

Nae Mbunge wa Kasulu Vijijini ,Vuma Holle alisema Suala hilo la Hifadhi ya poli la Kagerankanda amekwasha lipeleka Wizarani na Wizara inalitambua suala hilo linasubili sheria zikamilike na liweze kutatuliwa wananchi waweze kunufaika na maeneo yao.

Alisema Wananchi wa Kasulu ni wengi sana na maeneo hayo hayawatoshi waongezewe mipaka Waweze kulima kwakuwa Wengi wao wanategemea kilimo jambo ambalo linaweza kuwa suruhisho kwa Suala hilo ni kuongeza mipaka ya Wakulima iliwaweze kulima.

Aidha Holle alimuomba Rais kulitatua Suala hilo la Wananchi kuchomewa mazao yao suala linaloweza kuhatalisha hali za Wananchi Wa Wilaya ya Kasulu hali inayoweza kupelekea njaa katika Wilaya hiyo.

No comments: