Saturday, January 21, 2017

NAIBU MEYA ILALA AWATAKA WENYE VIWANDA KULINDA MASLAHI YA WAFANYAKAZI



Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala , Omary  Kumbilamoto akizungumza na wadau wakati wa uzinduzi wa kiwanda cha dawa cha ZENUFA.



Mkurugenzi wa kiwanda cha Zenufa Laboratories Ltd,Hitesh Upret akizungumza na wadau wa wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho na muonekano wa alama mpya.



Afisa Tarafa Ilala , Edita Samson akizungumza kwa niaba ya mkuu wa Wilaya ya Ilala wakati wa uzinduzi wa nembo mpya ya dawa ya Zenufa.


Mkurugenzi mtendaji wa bohari ya Dawa nchini(MSD), Laurean Rugambwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa nembo mpya ya dawa ya Zenufa.


Na Humphrey Shao, Globu ya jamii

NAIBU Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti, Omary Kumbilamoto amewataka wenye viwanda kulinda maslahi ya wafanyakazi kabla ya serikali kuingilia kati.
Kumbilamoto amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya uzinduzi wa nembo mpya ya kiwanda cha dawa cha ZENUFA kilichopo kata ya Kipawa.

“tunashukuru kwa ujenzi wa kiwandahiki na kuweza kuongeza ajira kwa vijana wetu kama ilivyo sera ya serikali kuwa nchi ya viwanda lakini kikubwa ninacho waomba muweze kuangalia maslahi ya wafanyakazi kuliko kusubiri msumbuliwe na serikali”amesema Kumbilamoto.

Ametaja kuwa itakuwa jambo la aibu kuona mkuu wa mkoa au Meya ama Naibu Meya anakuja tena kiwandani hapa kwa ajili ya kuja kusuluhisha mgogoro wa kiwanda na wafanyakazi.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa boahari ya dawa nchini, Raurean Rugambwa amesema kuwa serikali imejipanga kuakikisha inasaidina na wawekezaji wa viwanda vya dawa kwa kuwa hakikishia uakika wa soko.

Ametajakuwa kwa sasa serikali yako imekuwa ikiagiza dawa kwa asilimia 90% kutoka nje ya nchi kutokana na upungufu wa viwanda vya dawa hapa nchini.

Hivyo amewataka wawekezaji kujitokeza katika uwekezaji mpya wa viwanda vya dawa katika mpangomaalumu wa mashirikiano na serikali(PP).


wananchi na wadau waliofika katika uzinduzi huo wakifatilia kwa makini matukio yanayoendelea

Mkurugenzi wa kiwanda cha Zenufa Laboratories Ltd,Hitesh Upret akiwaonyesha wageni waliofika kiwandani hapo sehemu ya kiwanda hicho ambacho kinazalisha dawa aina ya Zenufa.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Dar es Salaam,Ramadhani Madabida akizungumza jambo na mmoja wa watumsihi kutoka MSD waliofika katika uzinduzi wa kiwanda hicho.

No comments: