Thursday, January 26, 2017

MAONESHO YA KILIMO YA AGRI TECH YAWAVUTIA WENGI MKOANI ARUSHA



Mtaalamu wa Mawasiliano wa taasisi ya Agriculture Markets Development Trust(AMDT),Al-amani Mutarubukwa(kulia)akitoa maelezo kwa Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro(wa pili kulia)kuhusu taasisi hiyo inayowajengea uwezo wakulima katika mazao ya Ufuta na Mahindi katika mikoa mbalimbali nchini. 
Meneja wa Kampuni ya Monsanto nchini,Frank Wenga(kulia)akizungumza na wakulima waliofika kwenye maonesho hayo kujifunza mbinu za kilimo chenye tija. 
Wakulima kutoka maeneo mbalimbali wakipata elimu ya matumizi ya kilimo bora na chenye tija. 
Wakulima wakipata maelezo kutoka kwa wataalamu namna ya kupata mazao bora 
Mmoja wa wakulima wakiangalia mazao yaliyostawisha kwa kufuata kanuni za kilimo 
Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro akifungua maonesho ya siku mbili ya kimataifa unaofanyika kwenye viwanja vya taasisi ya Utafiti wa Kilimo Selian(Sari)jijini Arusha. 
Sehemu ya mitambo iliyopo tayari kwaajili ya wakulima. 


No comments: