Thursday, January 26, 2017

GAZETI LA HABARILEO LAADHIMISHA MIAKA 10 TANGU KUANZISHWA KWAKE,WAZIRI NAPE ALIPONGEZA KWA KUIELIMISHA JAMII

Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi (kushoto) na Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa, Dk Selemani Sewange wakiweka saini makubaliano ya kukuza lugha ya kiswahili kupitia gazeti la Habari Leo wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka kumi ya gazeti hilo, jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia (kutoka kushoto waliosimama) ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, Naibu Mhariri Mtendaji wa TSN, Tuma Abdallah, Kaimu Mhariri wa  Habari Leo, Nicodemus Ikonko na Mwanasheria wa TSN, Mwadawa Sakware  (kulia)
 Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi (kushoto) na Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa, Dk Selemani Sewange wakikabidhiana makubaliano ya kukuza lugha ya kiswahili kupitia gazeti la Habari Leo wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka kumi ya gazeti hilo, jijini Dar es Salaam. 
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye,akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya miaka 10 ya gazeti la HabariLeo,iliyofanyika leo katika uwanja wa Taifa,jijini Dar.Waziri Nape alisema kuwa Gazeti hilo lililoanza kuchapishwa rasmi Desemba 21, 2006,limekuwa na  mchango mkubwa sana katika juhudi za kuepuka migawanyiko ya kisiasa nchini, na kuimarisha juhudi za kuendeleza umoja wa kitaifa. 

"Na hili likiwa ni mojawapo ya malengo ya msingi na kusudio la kuanzishwa kwa Gazeti la HabariLeo na kwa kweli niwapongeze kwa namna mlivyolifanya kwa kiwango cha juu kabisa,Muda wa miaka 10 sio mdogo kwa uhai wa gazeti hasa kutokana na ushindani mkubwa na changamoto mbalimbali zinazoikabili tasnia ya habari hapa nchini na duniani kote.",alisema Waziri Nape.
 Mgeni rasmi,Waziri Nape akizindua bahati nasibu ya watoto waliozaliwa desemba 21,2006,anaeshuhudia pichani kulia Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi 
 Uongozi wa TSN ukimkabidhi zawadi ya Picha Waziri Nape 
 Muda wa Cheers kwa meza kuu
 Chiaazzzzz
 Waziri Nape akiwasha mishumaa iliyowekwa kwenye keki maalum kwa ajili ya maadhimisho hayo
 Waziri Nape pamoja na uongozi wa TSN ,Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi (kushoto) na Naibu Mhariri Mtendaji wa TSN, Tuma Abdallah (kulia) kwa pamoja wakikata  keki maalum kwa ajili ya maadhimisho hayo
 Waziri Nape akiongoza meza kuu kukata  keki maalum kwa ajili ya maadhimisho hayo. 
 Waziri Nape akimlisha keki Mhariri Mtendaji wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi

 Waziri Nape akionesha umahiri wake wa kupiga gitaa na kuimba ikiwa ni sehemu ya kuonogesha maadhimisho ya miaka 10 ya gazeti la Habarileo





Wafanyakazi wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN) na wageni mbalimbali wakifuatilia matukio ya maadhimisho ya sherehe za miaka kumi ya gazeti la Habari Leo, yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.




















No comments: