Wednesday, December 21, 2016

Yaliyojiri Katika Vituo Mbalimbali vya Televisheni

SIMU TV : Serikali yasuluhisha mvutano wa pande zinazozalisha umeme katika kituo cha kufua umeme cha Nyakato jijini Mwanza; https://youtu.be/j6KzX3qhWG8

SIMU TV :  Watu wanne wamefariki dunia wakiwemo askari wawili wa jeshi la polisi baada ya gari aina Toyota Alphard kuacha barabara na kupinduka mkoani Dodoma;https://youtu.be/yl63uTgLTf8

SIMU TV : Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli akutana na kufanya mazungumzo na viongozi watatu wapya wa CCM aliowateuwa hivi karibuni; https://youtu.be/RwxtqP7nOsk

SIMU TV : Mkuu wa mkoa wa Songwe amsusha cheo afisa elimu kata ya Gua kwa kushindwa kudhibiti tatizo la utoro wa walimu https://youtu.be/iK2rAcS_Q2I

SIMU TV : Baadhi ya wafanyabiashara wa Kariakoo jijini Dar es Salaam wakiri kufanya biashara katika mazingira ya hatari; https://youtu.be/BpjegRWtILM

SIMU TV : Mkulimwa wa zao la Mwani kutoka visiwani Zanzibar alalamikia kuhusu bei ya zao hilo kuwa ndogo; https://youtu.be/dzJr_asgi-g

SIMU TV : Shirika la hifadhi ya jamii NSSF kanda ya Ilala Dar es Salaam yatoa msaada wa mashuka na dawa katika hospitali ya Amana; https://youtu.be/52SSvRCklqI

SIMU TV : Serikali imewataka  wasanii kurasimisha kazi zao ili kupata takwimu sahihi ya kazi zao; https://youtu.be/iAQ9OYyoEHU

Tbc:Uongozi wa klabu ya Yanga wakanusha juu ya taarifa zilizoenea kuwa wachezaji wa klabu hiyo wamegoma kufanya mazoezi; https://youtu.be/ZYomYlQQOVc

SIMU TV : Idara ya uhamiaji imesema inalifanyia uchunguzi suala la wachezaji wawili wa Simba kucheza bila ya vibali  vya kazi; https://youtu.be/NY7aaqlWC54

SIMU TV : Timu ya taifa ya vijana wa umri chini ya miaka 14 yavunja kambi yake baada ya kumaliza michezo yake ya kirafiki; https://youtu.be/DWVI9emwgF4

SIMU TV: Serikali imewakumbusha waajiri wote nchini kuwataka wafanyakazi wao kupeleka fedha zao katika mifuko ya hifadhi ya jamii kama sheria inavyowataka; https://youtu.be/cYw49Y0zNRE

SIMU TV : Upatikanaji wa maji safi na salama katika wilaya za Newala na Tandahimba mkoani Mtwara bado changamoto inayohitaji kutatuliwa; https://youtu.be/qi9VvZy-WyQ

SIMU TV : Naibu waziri Luhaga Mpina amevipiga marufuku viwanda vilivyoko eneo la Keko wilayani Temeke kuacha kutiririsha maji machafu katika makazi ya watu; https://youtu.be/-6b2BaZv2GM

SIMU TV : Mkuu wa wilaya ya Kakonko Hosea Ndagala, ameonya tabia ya baadhi ya wananchi kuharibu vyanzo vya maji na kupekelea kukauka kwa vyanzo hivyo; https://youtu.be/4ti8W-iIU_E

SIMU TV : Benki ya maendeleo Afrika AFDB imeipatia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu wa shilingi Bilioni 360 kwa ajili ya kusaidia bajeti 2016/2017; https://youtu.be/cnvl6Z2AerY

SIMU TV : Mkuu wa wilaya ya Rufiji Juma Njwayo amewataka vijana waliopatiwa maarifa ya kilimo kwa vitendo wilayani humo kutumia ujuzi huo kujikwamua kiuchumi; https://youtu.be/uyM-DiDbLvg

SIMU TV : Chama cha mpira wa miguu mkoani Geita kinatarajia kufanya uchaguzi hapo kesho ili kuwapata viongozi wapya wa kuongoza kwa miaka minne ijayo; https://youtu.be/ggSC_b_pZfU

SIMU TV : Baada ya timu ya Ndanda Fc kufungwa mabao 2 na Simba, wadau wa timu hiyo wameombwa kuendelea kuisaidia kiuchumi ili waweze kufanya vizuri; https://youtu.be/djCwCaZx-sY

SIMU TV : Shirikisho la riadha nchini limeanzisha kisheria vyama vya riadha kwa ngazi za wilaya ili kuwezesha usajili wa wanariadha kuanzia ngazi za wilaya; https://youtu.be/Qrog3lg_Luk

No comments: