Thursday, December 1, 2016

TTCL yawakumbuka wanafunzi wa vyuo huduma za intaneti

Kaimu Mkurugenzi wa Biashara Kanda ya Dar es Salaam, Jane Mwajalebela akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 'Business School' (UDBS). 
Kaimu Mkurugenzi wa Biashara Kanda ya Dar es Salaam, Jane Mwajalebela akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 'Business School' (UDBS) (hawapo pichani). 
Kaimu Mkurugenzi wa Biashara Kanda ya Dar es Salaam, Jane Mwajalebela akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 'Business School' (UDBS) (hawapo pichani). 
Baadhi ya wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 'Business School' (UDBS) (hawapo pichani). 
Semina ikiendelea kwa wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 'Business School' (UDBS) (hawapo pichani). Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Biashara Kanda ya Dar es Salaam, Jane Mwajalebela. 
Baadhi ya wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 'Business School' (UDBS) wakisajili laini za wanafunzi ambazo zinajulikana kwa jina la Boompack. 
Baadhi ya wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 'Business School' (UDBS) wakisajili laini za wanafunzi ambazo zinajulikana kwa jina la Boompack.

KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) imetoa laini maalumu za simu za mkononi kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo zitakazokuwa na gharama nafuu za matumizi ya mtandao wa intaneti na ofa mbalimali za matumizi ya simu kuwawezesha wanafunzi kutumia mtandao kwa masomo yao. 

Akizungumzia ofa hiyo maalum iliyotangazwa kwenye semina kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Biashara Mlimani wa mwaka wa kwanza, Kaimu Mkurugenzi wa Biashara Kanda ya Dar es Salaam, Jane Mwajalebela alisema ofa hiyo kwa wanafunzi wa chuo imetolewa baada ya TTCL kusikiliza ombi la wanafunzi juu ya kupunguziwa gharama hasa kwenye intaneti kwa kuwa hutumia mtandao huo kujipatia masomo.

 Bi. Mwajalebela alisema laini hizo kwa wanafunzi ambazo zinajulikana kwa jina la 'Boompack', ambapo wanafunzi wa chuo watakuwa na fursa ya kupata huduma za vifurushi vya bei nafuu, ujumbe mfupi wa simu 'SMS' za kutosha na muda wa maongezi ambao kiujumla utarahisisha huduma kwa matumizi yao.

 "leo na Hivyo basi, tunapenda kuwatangazia kuwa TTCL inatoa laini za wanafunzi ambazo zinajulikana kwa jina la Boompack, wanafunzi wanafursa ya kupata huduma za vifurushi vya bei nafuu, SMS za kutosha na muda wa maongezi. Laini hii ni maalumu kwa wanafunzi na tumeanzisha ili kutoa fursa kwa wanafunzi kutumia intaneti kwa ajili ya kushughuli za kimasomo na kuimarisha mawasiliano miongoni mwa wanafunzi. 

Pia, tumeongeza radha zaidi wanafunzi waweza kuchagua vifurushi vya Siku, Wiki na Mwezi. Zaidi na zaidi, Kwa wanafunzi watakajiunga na kifurushi chochote watapata fursa ya kuperuzi facebook, Instagram, Whatsapp na E-mail Bure," alisema Bi. Mwajalebela. Aliongeza kuwa TTCL inaamini kuwa wanafunzi watatumia huduma hiyo kikamilifu ili kuimarisha mawasiliano miongonu mwao, kutumia intaneti kwa ajili ya kutafuta taarifa za kimasomo, kupata taarifa za maendeleo na kutumia fursa hiyo kuongeza wigo wa maarifa kwa kushirikiana na vyuo vingine ndani na nje ya Tanzania. 

Awali ya yote, naomba kuchukua nafasi hii kushukuru sana Uongozi wa DARUSO- University of Dar es salaam Business School (UDBS) kwa kutualika TTCL ili tuweze kushiriki nanyi kwenye tukio la leo la kuwakaribisha wanafunzi ambao wamejiunga Mwaka wa Kwanza. 

Kwa niaba ya Menejimenti ya TTCL, inapenda kuwapongeza kwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam, tunaamini ni fursa yenu pekee ambayo mnapaswa kuitumia kikamilifu ili muweze kujijenga wewe binafsi na kutumia elimu hiyo kujenga Taifa letu. Pia, tunafarijika sana kuona wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kupitia DARUSO-UDBS kutuamini na kutambua mchango wa TTCL katika kuimarisha mawasiliano ndani na nje ya mipaka ya Tanzania, kukuza uchumi na kuongeza kasi ya maendeleo nchini. 

Tunaimani kuwa wanafunzi na uongozi wa Chuo mtakuwa mstari wa mbele katika kutumia huduma za Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Alisema Kampuni ya Simu Tanzania(TTCL) ilianzishwa mwaka 1994 ambapo inamilikiwa na serikali kwa asilimia 100. Kampuni hii inatoa huduma za mawasiliano ya simu ya mezani, simu za mkononi na intaneti kwa wateja wa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. Kampuni hii imekuwa mhimili mkuu wa mawasiliano katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara. 

Na hii inatokana na uwezo wake wa kuunganisha nchi za jirani kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ambapo TTCL ndio Msimamizi kwa niaba ya Serikali. Nchi hizo ambazo zimeunganishwa kwenye Mkongo wa Tafa ni pamoja na Uganda, Rwanda, Burundi, Kenya, Malawi na Zambia. Aidha, Kampuni ya Simu Tanzania(TTCL) inamiliki Kituo cha Mawasiliano cha Intaneti- TTCL IP-Pop ambacho kinatoa huduma ya intaneti kwa wateja kutoka ndani ya nchi na nje ya mipaka ya Tanzania. Kituo hiki kimekua msaada mkubwa, hivi sasa Intaneti inapatikana hapa hapa Tanzania hakuna tena haja ya kwenda kununua intaneti Ulaya au kwingineko. Alisema kuwa TTCL ni kampuni pekee yenye mtandao ambao umeenea nchi nzima, hivyo kutoa fursa kwa taasisi za Umma na Binafsi kutumia miundombinu hiyo kukuza biashara na kuongeza ufanisi katika kutoa huduma kwa wananchi. 

TTCL imefanikisha kuuganisha Taasisi za Umma na Binafsi katika Mkongo wa TTCL ambao umeunganishwa katika Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano; wateja hao ni pamoja Taasisi za fedha-Benki, watoa huduma za Afya, watoa huduma za elimu, watoa huduma za Mawasiliano (service providers), watoa huduma za usafiri, wafanyabishara wadogo na wakati (SMEs). 

Mwaka 2014, Kampuni ilianza kutekeleza mkakati kabambe wa kuleta mageuzi ndani ya kampuni, kuongeza uwajibikaji, kukuza biashara na kuboresha miundombinu ya mawasiliano. Mkakati huu umekuwa na manufaa kwa Kampuni kutokana na kufanikiwa kuboresha huduma za simu za Mkononi. Hivi sasa Kampuni hii inatoa huduma za simu za mezani, simu za mkononi na huduma ya intaneti. Kwa simu za mkononi ambazo vijana wengi wanatumia zaidi,

 TTCL inatoa huduma hiyo kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya 4.5G ambayo inatoa intaneti yenye kasi zaidi, bei nafuu na bora zaidi. Pia, wateja wetu wanapata fursa ya kupiga simu kwa bei nafuu zaidi. Huduma hii tumeanza katika jiji la Dar es salaam na tuko kwenye mchakato wa kukamilisha huduma hiyo katika jiji la Mwanza, Arusha Mbeya na Dodoma pamoja na mikoa mingine itafuata.

No comments: