Friday, December 16, 2016

SIKU YA KWANZA YA SAFARI YA WANAHABARI NA ASKARI WA JESHI LA ULINZI (JWTZ) KUPANDA MLIMA KILIMANJARO KUSHEREHEKEA MIAKA 55 YA UHURU WA TANZANIA BARA

Waandishi wa Habari walioshiriki changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara wakinyanyua kuashiria kuanza safari hiyo atika lango la Marangu.
Safari ya kupanda ikaanza katika lango la Marangu majira ya saa 5 asubuhi kila mmoja akiwa na nguvu za kutosha na shauku ya kutzama madhari ya Mlima Kilimanjaro ambao siku ya kwanza safari inaanza kwa kupita katika msitu mnene.
Wapandaji waliokuwa wamevalia nguo za kuzuia baraidi mapema wakati safari ya kupanda mlima inaanza baadae kidogo kidogo walilazimika kuzipunguza kwa sababu pindi unapotembea joto la mwili pia huongezeka.
Safari ya kupanda mlima kwa kundi hili la Wanahabari na Askari wa jeshi la Ulinzi (JWTZ) wakiongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu,George Waitara lilikuwa pia na ulinzi wa kutosha. 
Safari ya kupanda vilima vidogo ndani ya Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro iliendelea.
Maeneo mengine yalikuwa ni ya Madaraja na Mito.
Hatimaye safari kafika eneo la Kisambioni ikiwa ni nusu ya safari ya kuelekea katika kituo cha Mandara ,eneo ambalo hutumika kwa ajili ya kupata chakula.
Baadae safari ya kuelekea kituo cha Mnadara ikaendeleo.
Maeneo mengine Washiriki walilazimika kupumzika kwa ajili ya kupata nguvu mpya ya kuendelea na safari.
Majira ya saa 12 jioni hatimaye Safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa siku ya kwanza ikafika katika kituo cha Mandara na washiriki wakapata nafasi ya kupata picha ya pamoja na kupumzika kwa ajili ya siku ya pili kuendele na safari ya kwenda kituo cha Horombo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya 
Jamii aliyekuwa katika safari hiyo.

1 comment:

moshy said...

SAFI SAAANA DIXON,ENDELEA KUWAHABARISHA WATANZANIA KUHUSU MLIMA WETU
NI THAWABU NA TUNU KUBWA SANA ALIYOTUPA MWENYEZI MUNGU
HATUWEZI KUUTANGAZA VYEMA MLIMA HUO BILA KUUJUA KWA KUUPANDA