Friday, December 30, 2016

MSAJILI WA HAZINA AKUTANA NA TAASISI ZA SERIKALI NA KUSAINI MAKUBALIANO YA UTEKELEZAJI WA MKAKATI WA MWAKA

Msajili wa Hazina Dk.Oswald Mashindano akikabidhiana na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya AICC Balozi Dk.Ladislaus Komba mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa mwaka kati ya Taasisi za Serikali na Zisizo za Serikali kupitia msajili wa Hazina.
Msajili wa Hazina Dk.Oswald Mashindano akizungumza jambo na baadhi ya wajumbe kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam(UDSM)na Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu vya Kitropiki Tanzania.(TPRI) wakati wa hafla ya makabidhiano ya makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa mwaka kati ya Taasisi za Serikali na zisizo za Serikali kupitia msajili wa hazina.
Msajili wa Hazina Dk.Oswald Mashindano akikabidhiana na mwakilishi kutoka Mfuko wa Umoja wa Dhamana ya Uwekezaji Tanzania mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa mwaka kati ya Taasisi za Serikali na Serikali kupitia msajili wahazina .Nyuma ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Umoja wa Dhamana ya Uwekezaji Tanzania Bw.James Washima.
Wajumbe mbalimbali kutoka Bodi yaWakurugenzi ya AICC na Mfuko wa Umoja wa Dhamana ya Uwekezaji  Tanzania wakimskiliza Msajili wa Hazina Dk.Oswald Mashindano (hayupo pichani) wakati wa makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa mwaka kati ya Taasisi za Serikali na Serikali kupitia msajili wa hazina.
MsajiliwaHazinaDk.Oswald Mashindano akikabidhiana na mwakilishi kutoka Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu vya Kitropiki  Tanzania (TPRI) mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa mwaka kati yaTaasisi za Serikali na Serikali kupitia msajili wa hazina.
Mhadhiriwa Chuo Kikuu cha Dar essaalaam Prof. Paramagamba Kabudi akitia saini mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa mwaka kati yaTaasisi za Serikali na Serikali kupitia msajili wa hazina leo Jijini Dar esSalaam.Kushoto kwake ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar esSalaam Profesa Rwekaza Mukandara


PichanaDaudiManongi-MAELEZO.

No comments: