Monday, November 21, 2016

Uchaguzi Mkuu Marekani : NEC yatoa somo, Watanzania wajifunze kuheshimu Mamlaka

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC)
Bw. Kailima Ramadhani
Na Margareth Chambiri – Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani amesema jambo kubwa ambalo watanzania wanapaswa kujifunza kutokana na Uchaguzi wa Marekani uliomalizika hivi karibuni ni kwa wananchi kuheshimi mifumo ya Uchaguzi.

 Mkurugenzi Kailima ametoa kauli hiyo ikiwa ni tathimi yake kuhusu uchaguzi huo wa Marekani na namna ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakihoji kuhusu ucheleweshaji wa kutangaza matokeo ya uchaguzi unaofanywa na Tume ikilinganishwa na ilivyofanyika nchini Marekani.

Akizungumza mwishoni mwa wiki katika kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa na Kituo cha Redio cha Clouds FM, Kailima amesema siyo sahihi kulinganisha uchaguzi wa Marekani na Tanzania, akitolea mfano sekta ya mawasiliano ambayo ni muhimu katika kusafirisha vifaa na taarifa mbalimbali za uchaguzi inavyokabiliwa na changamoto.

Amesema watanzania na hasa Wapiga kura wengi wanaishi maeneo ya vijijini ambayo baadhi yake hayafikiki kwa urahisi na kwamba haiwezekani Tume ikatangaza matokeo bila kuhakikisha kuwa kila kura imehesabiwa ikiwemo ya yule mwananchi wa kijijini.

Amebainisha kuwa yapo mambo ya msingi ambayo watanzania wanapaswa kujifunza kutokana na Uchaguzi wa Marekani, kubwa ikiwa ni hatua ya kuheshimu mifumo ya Uchaguzi sambamba na Mamlaka zinazosimamia chaguzi hizo.

Ametolea mfano wa uvumilivu katika kusubiri matokeo na Wagombea kuheshimu matokeo yanayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa sheria kwani hata pale ambapo anayeshindwa hakuridhika bado anaweza kupinga matokeo kwa kufuata taratibu zilizopo kisheria.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo amesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi inakamilisha Mwongozo wa Utoaji wa Elimu ya Mpiga Kura wa 2015-2020 ili iweze kuzishirikisha Asasi za Kiraia, Taasisi au Vikundi mbalimbali vya Watu wanaotaka kutoa Elimu hiyo.

Kwa mujibu wa Bwana Kailima Tume imo katika hatua za mwisho za kupitia Rasimu ya Mwongozo wa Elimu ya Mpiga Kura kwa ajili ya kuupitisha uweze kutumiwa na Wadau mbalimbali wa Uchaguzi.

Amesema pamoja na hatua ya Tume ya kuanza kutoa Elimu ya Mpiga Kura mapema kuliko ilivyozoeleka na wananchi, inakusudia kupanua zaidi wigo wa utoaji wa Elimu hiyo kwa kuwashirikisha wadau wengi zaidi wakiwemo Viongozi wa Dini.

Bwana Kailima amesema Tume kupitia kwa Mwenyekiti wake Mheshimiwa Jaji (Mstaafu) Damiani Lubuva baadaye mwezi huu itatoa taarifa rasmi kwa ajili ya kuzialika Taasisi na Asasi za Kiraia zinazotaka kutoa Elimu ya Mpiga Kura kuwasilisha maombi yao kwa ajili ya kupatiwa kibali rasmi cha kutoa Elimu ya Mpiga Kura.

Aidha Mkurugenzi huyo wa Uchaguzi amevitaja vigezo vya kupatiwa kibali kwa ajili ya kutoa Elimu ya Mpiga Kura kuwa ni pamoja na Cheti cha Usajili, Asasi au Taasisi kuwa imefanya kazi nchini kwa kipindi kisichopungua miezi sita pamoja na kuwasilisha majina ya watendaji wa juu wa Taasisi au Asasi husika.

Akizungumzia kuhusu tathmini ya zoezi hilo linaloendelea kufanywa na Tume yake, Bwana Kailima  Halmashauri amesema limekuwa na mafanikio makubwa na anaamini kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa Uchaguzi kutawezesha wananchi wengi kufikiwa na Elimu hiyo na kwamba Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 hakutakuwa na malalamiko na badala yake zoezi la uchaguzi litakuwa rahisi.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi tayari imeanza utekelezaji wa zoezi la Utoaji wa Elimu ya Mpiga Kura ambapo imeshiriki katika maonesho mbalimbali yakiwemo ya Biashara ya Kimataifa na yale ya Wakulima pamoja na kutembelea na kutoa Elimu ya Mpiga Kura katika shule kadhaa za Sekondari hapa nchini. 

1 comment:

Tiba asili said...

UTAJIRI AU FEDHA ZA NDAGU AU MAJINI KWA MUDA MFUPI MPAKA MASAA 48(Siku 2) POPOTE ULIPO.

(Kwanza kabisa nataka kukwambia kwamba hakika utajili ni azina kutoka kwa mwenyezi mungu na pia kuna viumbe alio wapa mamlaka na nguvu ya kumiliki mali)

MPAKA MASAA 72(SIKU3) PAPO HAPO KWA MASHARTI MAALUM KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......

KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA

kwa maelezo kamili piga namba +255 742162843

(KWANINI USUMBUKE,HACHA KUTANGATANGA, NA MAISHA NI MAFUPI PUUZA UONGOFU WA KUWA MTU KUWA TAJIRI NI DHAMBI WAKATI AKUAMBIAE YEYE NI TAJIRI (Tumia ufahamu kujinasuaUTAJIRI WA NDAGU(MASHARTI) NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......

KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO TUNAPITIA MENGI ILI TUWEZE KUFANIKIWA LAKINI WENGI WETU KUNA MAMBO MACHACHE SANA WENGI WETU TUNAYADHARAU NA KUMBE NDIO CHANZO CHA MAFNIKIO YETU.

NAITWA DR, MDIRO piga 0742162843. KAMA UNAITAJI PESA ZA MAJINI AU NDAGU YA MALI AU ULINZI KWA MALI YAKO
(HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)
MATIBABU MENGINEYO NI KAMA UTULIVU KATIKA NDOA, AU KUMVUTA UMPENDAE, KUONDOA MIKOSI, MABALAA, KUOSHA NYOTA, KUITAMBUA NYOTA YAKO NA ASILI YA KAZI YAKE, KAMA UNASUMBULIWA NA MAJINI MAHABA NA SHIDA YA UZAZI.

NIPIGIE 0742162843. KIKUBWA NI KUSIKILIZA NA KUFATA MASHARTI. ANGALIZO USITUME SMS PIGA NA UWE NA NIA.

(kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
1. uwe una umri wa miaka 18+
2. uwe tayari kupokea masharti yote
3.uwe na uwezo wa kutunza siri
4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO
SAFARI YAKO YA MAFANIKIO UTAJIRI NA RIZIKI ZAKO ZIMESIMAMA NA KUZINASUA UWEZE KUSONGA MBELE SOMA KWA UMAKINI UWEZE KUIJUA SIRI HII.

HAYA NI MAMBO 7 YAKUZINGATIA KATIKA SAFARI YAKO YA MAFNIKIO

i) Wazazi wako wakiwa wamekulea mpaka ukawa mkubwa wafumbua macho unawaona akikisha usiwafanye wakajuta kukuzaa asilimia kubwa wazazi wanakuwa na tabu sana ila zile tabu zao ndio zinazokufanya wewe una aminiwa na watu na unaeshimika na kujieshimu

Kwaiyo jitahidi sana kuwa nao vizuri kuna wengi maisha yao wanaishi kwa shida chanzo ni utofauti baina ya wazazi wao

Ukiona wazazi wako wanatabu sana usiwajibu vibaya wewe kaa nao mbali ila wape majukumu yao unacho fanya kuwaona nakurudi ulipo apo utaona mambo yako yatakuwa vizuri sana

ii) JAMBO LA PILI
Akikisha unatunza uzao wako yani ukijua ni mtoto ni wako basi jitahidi sana kutoa uduma ata kidogo ulicho nacho lakini udumia usiache uzao wako unateseka na njaa wewe una kula maisha aisee fahau

Kila mtoto wako anavyo kuwa ndio mambo yako yanaaribika usipo udumia kwaiyo ukiwa waitaji kufanikiwa zaidi jali uzao wako

iii) JAMBO LA TATU
ukiwa umeoa au umeolewa usitoe talaka au kuomba talaka kabla mwenzio ayupo tayari kwa muda huo fahamu ukiomba talaka au akikupa talaka bila bila sababu ya msingi yeye tu ana matamanio ya kidunia basi anamuda atapoteza muelekeo wa maisha yake

iv) UKIWA WAPATA PESA
ukiwa wapata pesa alafu utoi sadaka basi kufikia kwenye ukuu utachelewa sana mana mana pesa badala ya kutoa kwa iyari yako utatoa kwa matatizo kwaiyo jitahidi icho icho kidogo toa sadaka kwa wenye uitaji

v) USIMZULUMU MTU
kama wataka kufika mbali kwenye mafanikio yako usimzulumu mtu ata kwa uchache wa kitu usifanye ivyo itakugarimu kiasi kikubwa

vi) USIZARAH MILA
ukiwa kwenu kuna mambo ya mila mzimu tambiko jitahidi kufatilia sana aya mambo yanarudisha nyuma sana usipo yawahi mapema

vii)USIWE WA NAMNA
1)ikiwa ujafanikiwa jitahidi sana usiwe mvivu kufanya kazi usiwe muhuni usiwe mwenye chuki na asira zisizo za msingi usiwe na tamaa nyoa vizuri vaa nguo za eshima na usiige maisha ya watu.

KWA MAWSILIANO ZAIDI KUHUSU MATATIZO MBALIMBALI YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA, PETE MALI ZA NDAGU NA MAJINI N.K

DOKTA MDIRO Call/whatsup +255 742162843