Friday, November 11, 2016

TTCL yapeleka intaneti bure Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba (kulia) akimkabidhi kibao cha kuashiria huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi (kushoto) leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma hiyo. Huduma hiyo ina itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120. Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba (kulia) akimkabidhi kibao cha kuashiria huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi (kushoto) leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma hiyo. Huduma hiyo ina itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120.Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba (kulia) akimkabidhi kibao cha kuashiria huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi (kushoto) leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma hiyo. Huduma hiyo ina itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120. Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba (kulia) akimkabidhi kibao cha kuashiria huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi (kushoto) leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma hiyo. Huduma hiyo ina itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120.Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akizungumza katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma ya bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Huduma hiyo itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akizungumza katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma ya bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Huduma hiyo itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120.Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba (kulia) akizungumza katika hafla ya kampuni ya TTCL kukabidhi huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akifuatilia. Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba (kulia) akizungumza katika hafla ya kampuni ya TTCL kukabidhi huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akifuatilia.

   KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) leo imefunga huduma za mawasiliano ya intaneti bure katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) itakayowawezesha madaktari, wafanyakazi wengine, wagonjwa pamoja na wananchi wanaofika katika kituo hicho kupata huduma ya mawasiliano ya intaneti bure yenye kasi ya hali ya juu. 

 Akikabidhi huduma hiyo, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba alisema kampuni hiyo imetumia jumla ya shilingi milioni 120 kufunga huduma bure ya intaneti katika kituo hicho na itatolewa kwa muda wa mwaka mmoja ikiwa ni kuiwezesha taasisi hiyo kuendesha shughuli zake kwa ufanisi.

 Akifafanua zaidi Bw. Kindamba alisema huduma hiyo ambayo itagharimu shilingi milioni 10 kwa kila mwezi ambazo zitakuwa zikilipwa na TTCL ikiwa ni mchango wake kwa jamii na hasa kwa matibabu yanayofanyika katika kituo hicho itakuwa ikitolewa kwa teknolojia ya Wi-Fi bure kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Novemba 10, 2016 hadi Novemba 10, 2017.

 "Kwa kuzingatia umuhimu wa sekta ya afya na kazi kubwa inayofanywa na Taasisi hii, TTCL tumetoa intaneti yenye kasi hadi kufikia spidi ya 100Mbps, spidi hii itasaidia kuongeza uwajibikaji katika kutoa huduma kwa wananchi, kuimarisha mawasiliano miongoni watumishi wa JKCI na nje ya Taasisi, kupashana habari za kitabibu na kubadilishana taarifa za kitabibu miongoni mwa wataalamu kutoka hospitali za ndani na hospital za nje ya mipaka ya Tanzania," alisema Kindamba. 

 Alisema mbali na huduma hiyo TTCL imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mawasiliano ya uhakika yanatumika katika sekta ya afya ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na tayari imefanikiwa kuunganisha hospitali za rufaa za Mkoa wa Dar es salaam kupitia Mkongo wa TTCL ambao umeunganishwa kwenye Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. 

 Aidha alizitaja hospitali nyingine zinazonufaika na huduma ya mawasiliano hayo ni pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili, Hospital ya Amana, Hospitali ya Mwananyamala, Hospitali ya Temeke, Hospitali ya Bagamoyo, Hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyopo Mkoa wa Kilimanjaro na Hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyopo mkoani Mwanza. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akizungumza katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma ya bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Huduma hiyo itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akizungumza katika hafla ya Kampuni ya TTCL kukabidhi huduma ya bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Huduma hiyo itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120.Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba akizungumza katika hafla ya kampuni ya TTCL kukabidhi huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo jijini Dar es Salaam. Huduma hiyo ina itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120. Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw. Wazir W. Kindamba akizungumza katika hafla ya kampuni ya TTCL kukabidhi huduma bure ya intaneti ya teknolojia ya Wi-Fi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo jijini Dar es Salaam. Huduma hiyo ina itakayotolewa kwa mwaka mmoja inagharimu shilingi milioni 120.

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akitoa shukrani zake mara baada ya kukabidhiwa huduma hiyo alisema TTCL inapaswa kutambua imetoa mchango mkubwa wa kuokoa maisha ya wagonjwa mbalimbali wanaopatiwa huduma katika taasisi hiyo. 

 Alisema kwa maendeleo ya sasa huduma za kitabibu zinatolewa kwa njia ya intaneti kwa wataalamu wa kituo kimoja kufanya mawasiliano na kituo kingine jambo ambalo limekuwa msaada mkubwa katika kutoa huduma hizo kwa wagonjwa na hata kukabiliana na changamoto ya baadhi ya wataalamu wa afya na vifaa vya matibabu.

 Alisema kwa JKCI huduma za intaneti sio kwa ajili ya starehe bali ni muhimu zaidi kusaidia madaktari katika kutekeleza majukumu yao, jambo ambalo kwa sasa watakuwa wakilipata muda wote wawapo eneo la kazi. Profesa Janabi aliongeza kuwa kiasi cha shilingi milioni 120 ambazo kituo cha JKCI ilipaswa kukilipa kwa gharama ya huduma hiyo sasa watakielekeza kwa wagonjwa zaidi ya 20 watakaofanyiwa upasuaji kwa fedha hizo ikiwa ni kutambua mchango wa TTCL katika kusaidia huduma za afya kwa jamii. 

"Ndugu Mkurugenzi kwa msaada wenu huu tambueni kuwa mmeokoa maisha ya wagonjwa takribani ishirini ambao hawana uwezo kulipia gharama za matibabu na sasa JKCI itawafanyia huduma za upasuaji kwa gharama mlizozitoa kwetu kutokana na mchango wenu kwa jamii...tutajitahidi kuwapa taarifa juu ya wagonjwa hao na idadi yake. Picha ya pamoja mara baada ya zoezi la makabiadhiano. Picha ya pamoja mara baada ya zoezi la makabiadhiano.

No comments: