Tuesday, November 8, 2016

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI


SIMU.TV: Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania limeitaka serikali kutosaini mkataba wa ubia wa uchumi kati ya nchi za Afrika mashariki na umoja wa Ulaya EPA. https://youtu.be/HulDwzsr8IU

SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Rukwa Zelothe Steven ameagiza kuwajibishwa watumishi wanne kutokana na kutowajibika kwa usafi wa vyoo vya kituo cha mabasi cha manispaa ya Sumbawanga. https://youtu.be/A-0IJWQO-_8
SIMU.TV: Mgodi wa kuchimba dhahabu wa GGM mkoani Geita umetumia zaidi ya milioni 700 kutengeneza madawati elfu kumi ili kumaliza tatizo la madawati mkoani humo. https://youtu.be/lQi9vCW5urs

SIMU.TV: Taasisi za haki za binadamu kutoka nchi za jumuiya ya Afrika mashariki zimekutana jijini Dar es Salaam ili kujadili namna ya kutatua changamoto za ukiukaji wa haki za binadamu. https://youtu.be/WLXrEQTLIes


SIMU.TV: Wakulima wa zao la korosho katika kata ya Matekwe wilayani Nachingwea wamemkataa mwenyekiti wa chama cha msingi cha Matekwe kutokana na kutokuwa na imani naye. https://youtu.be/6DnLP59q1_c

SIMU.TV: Shirikisho la wenye viwanda nchini CTI limezindua maandalizi ya tuzo ya rais ya mzalishaji bora wa mwaka ambayo hushindanisha wazalishaji mbalimbali nchini. https://youtu.be/CeqPcsfJtIs

SIMU.TV: Wadau wa michezo wamejitokeza kwenye mazishi ya aliyekuwa makamu mwenyekiti wa bodi ya ligi kuu Tanzania bara Said Mohamed aliyefariki dunia jana katika hospitali ya Agakhan. https://youtu.be/QpqgK0CBN7c

SIMU.TV: Ubalozi wa China kwa kushirikiana na kampuni ya ving’amuzi ya Startimes imesema unatarajia kuonesha filamu za kichina zilizotafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili ikilenga mahitaji ya watanzania. https://youtu.be/t9rhdoMaPXg

SIMU.TV: Wadau wa michezo kote nchini wameombwa kumsaidia mwanamichezo Arthur Mwambeta aliyelazwa katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete kwa ajili ya Marathi yanayomsumbua. https://youtu.be/YDTKJA2vkU4

SIMU.TV: Wabunge wa Tanzania wameishauri serikali kutosaini mkataba wa ushirikiano kiuchumi kati ya Jumuiya ya Afrika mashariki na Jumuiya ya Ulaya; https://youtu.be/rTchKOh2lCU

SIMU.TV: Watu wanne wamekufa baada ya gari waliyokuwa wakisafiria aina ya Toyota Hilux kupasuka tairi na kupoteza muelekeo wilayani Muleba mkoani Kagera; https://youtu.be/DVE1-H8AQjc

SIMU.TV: Mwili wa aliyekuwa spika mstaafu Samuel Sitta unatarajia kuwasili nchini siku ya Alhamis ukitokea nchini Ujerumani ambako alifariki dunia; https://youtu.be/O2PeJ9Plfcw

SIMU.TV: Baadhi ya wakazi wilayani Urambo mkoani Tabora wamemzungumzia marehemu Samuel Sitta kuwa ni mtu aliyewatetea wanyonge; https://youtu.be/sYYE2mnVxR4

SIMU.TV: SUMA JKT litaanza kuetekeleza mpango wa kufuga samaki kwa kutumia vizimba katika bahari ya Hindi baada ya mpango huo kufanikiwa katika maziwa na mito nchini; https://youtu.be/_qwuoJ0m3l8

SIMU.TV: Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amefikishwa katika mahakamani ya hakimu mkazi mjini Arusha na kusomewa mashtaka mawili ya uchochezi; https://youtu.be/M8W4YMbGGs8

SIMU.TV: Benki ya Twiga Bankcorp imeanza kutoa baadhi ya huduma chini ya usimamizi wa benki kuu mpaka pale watakapopatikana wawekezaji wapya; https://youtu.be/xrzSzGPaOJo  

SIMU.TV: Mfumuko wa bei wa taifa umebaki pale pale kwa asilimia 4.5 kutokana na kasi ya upandaji wa bidhaa na huduma kulingana na mwezi uliopita; https://youtu.be/kSHdbxeE-MY

SIMU.TV: Taasisi ya ujasiriamali na ushindani imesema program ya kijana jiajiri itatekelezwa nchi nzima ili kuhamasisha vijana kujiajiri wenyewe; https://youtu.be/YphKGSUENio

SIMU.TV: Shirikisho la wenye viwanda nchini limezindua shindalo la tuzo za Rais za mzalishaji bora huku zawadi nono zikiandaliwa kwa ajili ya washindi; https://youtu.be/yNlzkLASVwk

SIMU.TV: Shirika la Utangazaji nchini TBC limezindua muswada wa tamthilia  mpya ya Kiswahili inayokwenda kwa jina la Closed Chapter; https://youtu.be/z1Tbu8IXJKs

SIMU.TV: Mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa klabu ya Azam na bodi ya ligi yamefanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar Es salaam; https://youtu.be/GHUmbwmx2Gs

SIMU.TV: Vyuo vikuu nane vya Elimu ya juu nchini vitafanya bonanza la michezo mwishoni mwa juma hili katika viwanja vya Mabibo; https://youtu.be/DEcO8oRnb_I

SIMU.TV: Katibu mkuu wa FIFA Fatma Samora atatembelea nchini Sierra Leone kwenda kushughulia mgogoro wa michezo katika chama cha soka nchini humo; https://youtu.be/FbwpFRHSShc

No comments: