Tuesday, October 11, 2016

UCHUMI WA ZANZIBAR UNAZIDI KUIMARIKA ASILIMIA 7

Mwashungi Tahir na Fatma Makame/Maelezo Zanzibar

Waziri wan chi ofisi ya makamo wa pili ya rais Mohammed Aboud Mohammed amesema uchumi wa Zanzibar     unazidi kuimarika kwa karibu ya asilimia saba na mfumuko wa bei bado upo kwenye tarakimu  moja na  pato la Taifa linazidi kukua.

Ametoa maelezo hayo  ofisini kwake Vuga wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi Serikali ya awamu ya saba kipindi cha pili cha uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohammed Shein.

Amesema katika awamu hii kwa ujumla harakati za uchumi zinaendelea vizuri na ishara zote za kuimarisha uchumi katika mwaka huu wa fedha zinatoa sura nzuri za mafanikio.

Akizungumzia  suala la Muungano amesema unaendelea kuimarika na  vikao mbali mbali vya watendaji wakuu wa pande mbili wakiwemo  mawaziri vimeshafanyika na Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ameshafanya vikao viwili vya kisekta kwa nia ya kutatua changamoto zilizopo.

Waziri Aboud ameelezea kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekamilisha kazi ya kuipandisha hadhi iliyokuwa Idara ya upigaji chapa na mpigaji chapa mkuu wa serikali na kuwa wakala wa serikali wa uchapaji.

Aidha amesema kazi ya kufunga mitambo mipya ya uchapaji imekamilika na mafundi wa kiwanda hicho wanaendelea kupatiwa mafunzo ili kuimudu teknolojia mpya ya mitambo hiyo ili kuongeza ufanisi  na kuongeza upatikanaji wa huduma bora na kwa wakati.

Sambamba na hayo Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais kupitia Tume ya kitaifa ya kuratibu na udhibiti madawa ya kulevya imepania kutoa athari za madawa ya kulevya kwa jamii.

Hivyo Tume hiyo imefanya kikao maalum na maofisa na wapelelezi wa Jeshi la Polisi wa Mikoa na Wilaya  za Unguja kilichoongozwa na mkuu wa Mkoa Mjini Maghribi kuweka mikakati dhidi ya uingizaji na usambazaji wa madawa ya kulevya .

Mh Aboud amesema ofisi yake inashirikiana na Ofisi ya ukaguzi na mdhibiti mkuu wa Serikali kuendesha zoezi la uhakiki wa wafanyakazi wa Ofisi ya Makamo ya Pili ya Rais na Taasisi zake ili kubaini wafanyakazi hewa.

“Katika zoezi hili imebainika kwamba Ofisi yetu hakuna wafanyakazi hewa  kama inavyobainika sehemu nyengine" alisema wazirihuyo.

Aidha amesema Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais bado itaendelea kufanya kazi kwa bidii , ufanisi na tija ili iweze kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesisitiza kuwa mambo muhimu ya kuzingatiwa hivi sa kwa nchi yetu ni kuimarisha uzalendo na kusimamia matumizi bora ya ardhi kwani watukishirikiano katika masulala hayo tutaweza kudumisha amani na upendo na kupiga hatua zaidi ya maendeleo. 
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed akitoa tarifa ya mafanikio ya Ofisi yake kuhusiana na utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi kwa kipindi cha pili cha uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohammed Shein Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar. 
 Wandishi wa habari wakifuatilia tarifa ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed alipokuwa na mazungumzo nao  Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed alipokuwa akijibu maswali ya wandishi wa habari katika Mkutano wake Ofisini kwake Vuga.Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

No comments: