Sunday, October 23, 2016

TIMU YA GOLF YA LUGALO YATESA MASHINDANO YA PWC TROPHY

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na jeshi la Kujenga Taifa Mh Job Masima aliyeshinda kwa Senior akipiga mpira wakati wa mashindano ya PWC Trophy yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 22 katika uwanja wa Golf wa jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Lugalo Jijini Dar Es Salaam.
Baadhi ya Watoto (Junior) wa Klabu ya Golf ya Lugalo walioshiriki mashindano ya PWC Jumamosi Oktoba 22 Jijini Dar es Salaam wa Pili Kulia ni Mshindi wa Kwanza wa Kundi hilo Almadius Simon wa Klabu ya Lugalo.
Wachezaji wa Golf kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh Job Masima, Dk Edmund Mndolwa aliyekuwa Mkuu wa majeshi Jenerali Mstaafu George Waitara na Balozi Clemence Sanga wakibadilshana mawazo kabla ya kuanza mashindando ya PWC yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 22 katika Uwanja wa Golf Lugalo Jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa Jumla wa mashindano ya PWC yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 22 Jijini Dar es Salaam Nicholous Chitanda wa Lugalo aliyeshika Vikombe akiwa katika Picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa Kushoto ni mwenyekiti wa Klabu ya Lugalo Brigedia Jenerali Michael Luwongo , wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa TGU Joseph Tango na wa pili kulia ni Msuya Mkurugenzi PWC .(Picha na Luteni Selemani Semunyu).

Na Luteni Selemani Semunyu JWTZ

Mchezaji wa Klabu ya Golf ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo Nicholous Chitanda imeibuka washindi wa Jumla katika mashindano ya wazi ya PWC Trophy yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 22 katika uwanja wa Golf wa Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Chitanda aliibuka na ushindi huo nakuwashinda wachezaji wengine zaidi ya 100 waliojitokeza kutoka Klabu zote Nchini baada ya kupata Mikwaju au Gross 74 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni Tisa na hivyo kuibuka na Mikwaju ya Jumla Net ya 65.

Katika Division A ushindi ulinyakuliwa na Isack wanyenche kutoka Klabu ya Arusha baada kupiga mikwaju 69 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni Tatu na hivyo kuibuka na ushindi kwa kupiga mikwaju ya jumla 66 na kufuatiwa na Juma Likuli wa Lugalo baada ya kupiga mikwaju ya jumla 68.
Kwa upande wa Division B mshindi ni Dk James Legg wa Lugalo baada ya kupiga mikwaju 84 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 13 na hivyo kuwa na mikwaju ya jumla 71 na kufuatiwa na Salum Mvita wa Dar es Salaam Gymkhana kwa mikwaju ya Jumla 71.

Division C kwa upande wake Mpiga Golf Reneir Kuhcmanu wa Lugalo aliibuka na ushindi katika kundi hilo baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 68 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 24 akifuatiwa na Kapten Amanzi Mandengule wa Lugalo pia baada ya kupata mikwaju ya Jumla 69 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 19.

Kwa upande wa Kundi la Wazee ama Senior Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh Job Masima alishinda kwa kupiga Mikwaju ya Jumla 75 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 18 akifuatiwa na Balozi Clemence Sanga aliyepiga mikwaju ya Jumla 78 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni 16.

Wanawake kwa upande wa kundi lao Chiku Elias wa Lugalo aliibuka na Ushindi kwa Mikwaju ya JUmla 76 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 10 na kufuatiwa na Vicky Elias wa Lugalo kwa mikwaju ya Jumla 78 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni Nane.


Katika Upande wa Wachezaji wa Kulipwa Nuhu Mollel wa Arusha aliibuka Mshindi ,watoto Junior Almadious Simon wa Lugalo aliibuka na Ushindi baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 70 na kwa upande wa Wachezaji wasaidizi au Cardes Hendrick Nyenza wa Lugalo aliibuka Mshindi kwa Mikwaju 78 akifuatiwa na Deo Hassan wa Lugalo.

No comments: