Tuesday, October 11, 2016

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA KONGAMANO LA NISHATI AFRIKA

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ( wa nne kutoka kulia) katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Maendeleo  ya  Afrika (AfDB), Ubalozi wa  Sweden na Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP).
 

Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano litakalokutanisha nchi mbalimbali za Afrika kwa ajili ya kujadili na kubadilishana uzoefu katika masuala ya Nishati linalotarajiwa kufanyika Aprili mwaka 2017. Hayo yameelezwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alipofanya kikao na wawakilishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC) Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Ubalozi wa Sweden na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akiongoza kikao kilichokutanisha wawakilishi kutoka kutoka Wizara ya Nishati na Madini,  Benki ya Maendeleo  ya  Afrika (AfDB), Ubalozi wa  Sweden na Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP). Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa  Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe.
 Wawakilishi kutoka Benki ya Maendeleo  ya  Afrika (AfDB), Ubalozi wa  Sweden na Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP), wakifuatilia maelezo  yaliyokuwa yanatolewa na  Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) katika kikao hicho.
 Wawakilishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Mkurugenzi Mkazi wa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (hayupo pichani) katika kikao hicho.

Mkurugenzi Mkazi wa na Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo akisisitiza  jambo katika kikao hicho.


 Mkurugenzi Mkazi wa  Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya  Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

No comments: