Tuesday, October 11, 2016

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

SIMU.TV: Makamu wa rais Samia Suluhu, amesema serikali imejipanga kuongeza huduma za afya nchini kwa kuongeza hospitali za rufaa; https://youtu.be/otSjb1EM2-Q

SIMU.TV: Waziri mkuu Kassim Majaliwa, amepokea zaidi ya shilingi milioni 600 kutoka kwa wadau mbalimbali ili kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera;https://youtu.be/WjmcIkotAY8

SIMU.TV: Rais wa Zanzibar Dr Alli Mohamed Shein, amefungua rasmi mkutano wa tano wa bunge la Afrika Mashariki na kuwataka wabunge kuharakisha ukuaji wa uchumi;https://youtu.be/8EbC_gTH9u8

SIMU.TV: Halmashauri ya manispaa ya Tabora, imebomoa tena nyumba za wananchi waliovamia na kujenga katika kiwanja cha shirika la utangazaji TBC ;https://youtu.be/WrTFkuFRuiY

SIMU.TV: Waziri wa ujenzi Prof Makame Mbarawa, amewataka wananchi kushirikiana na vyombo vya dola ili kufanikisha kuwakamata watu wanaohujumu  miundombinu ya barabara;https://youtu.be/HuO5JTX6AVU

SIMU.TV: Endelea kutazama sehemu ya hotuba ya Mwalimu Nyerere aliyozungumzia kuhusiana na uvamizi aliowahi kuufanya nduli Idd Amini wa Uganda mkoani Kagera;https://youtu.be/QWiyoHRp-OQ

SIMU.TV: Kampuni ya Bakhresa foods ina mpango wa kujenga kiwanda cha kusindika matunda katika eneo la kanda ya ziwa ili kuwasaidia wakulima wa matunda wa mikoa hiyo kupata soko; https://youtu.be/gBfCfk4h6dY

SIMU.TV: Naibu waziri wa fedha na mipango Dr Ashantu Kijaji, ameitaka benki ya kilimo TADB kutafuta fedha za kutosha ili kuwasaidia wakulima mikopo; https://youtu.be/waGuImTN4jQ

SIMU.TV: Mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF, umeendelea na mpango wake wa kunusuru kaya masikini kwa kutoa fedha katika kaya 204 visiwani Zanzibar;https://youtu.be/JvLMRw4odCY

SIMU.TV: Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF, limeitaka klabu ya Yanga kupeleka mkataba uliosainishwa na klabu ya Yanga ili kuruhusu timu hiyo kukodishwa kwa mwekezaji;https://youtu.be/dz7QljAROOs

SIMU.TV: Ligi kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea kutimua vumbi hapo kesho katika viwanja tofauti, huku vigogo wa ligi hiyo Yanga watakuwa uwanja wa Uhuru na wenzao Simba watakua huko jijini Mbeya; https://youtu.be/3G8TpV-kvGQ

SIMU.TV: Nahodha wa zamani na nguli wa timu ya AC Milan Paolo Maldini, amekataa kuwa mjumbe wa bodi katika timu hiyo kwa kile alichokisema kupoteza muelekeo kwa timu hiyo;https://youtu.be/yfGH1Ecl0yw
SIMU.TV: Makamu wa rais mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amezindua ujenzi wa majengo matatu yatakayotumika kwa ajili ya huduma za afya kwa akina mama na watoto jijini Dar es Salaam. https://youtu.be/phtLnrkz6to

SIMU.TV: Serikali imesema imebaini kuwepo kwa taasisi zaidi ya kumi na tano nchini ambazo zinaendesha semina za kuhamasisha ndoa za jinsia moja. https://youtu.be/ZH6ZBaKPkx8

SIMU.TV: Mkuu wa wilaya ya Kilombero amemuagiza mkurugenzi wa wilaya hiyo kuwachukulia hatua za kisheria wenyeviti ambao katika maeneo yao kuna watoto walioolewa wakiwa na umri mdogo. https://youtu.be/XZkgqgeHwfs

SIMU.TV: Katibu mkuu wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto awataka wasichana kujitambua ili kufanikisha vita ya ndoa za umri mdogo na mimba za utotoni.https://youtu.be/EWSC_oOnZAc

SIMU.TV: Waziri mkuu Kassim Majaliwa awahimiza wananchi na mashirika kuendelea kuwachangia waathirika wa tetemeko la ardhi. https://youtu.be/38G2PSPwB1k

SIMU.TV: Kampuni ya Bakheresa Foods imedhamiria kuongeza viwanda vya kusindika matunda ili kuongeza thamani kwa wakulima. https://youtu.be/7vwlRhAuaWI

SIMU.TV: Wakazi wa vijiji vya Mgao na Kisiwa katika halmashauri ya mkoa wa mtwara wametoa siku kumi na tano kwa mamlaka ya bandari TPA kuwalipa fidia kwa ajili ya maeneo yao yaliyochukuliwa. https://youtu.be/s6oOIlk8wV0

SIMU.TV: Serikali imeitaka benki ya mendeleo ya kilimo nchini kuwa mstari wa mbele kuhakikisha inafanikisha uwepo wa malighafi ya viwanda kwa kuwainua wakulima ambao ndio wazalishaji. https://youtu.be/d1HYgscGCI0

SIMU.TV: Wafanyakazi wa sekta binafsi na serikali nchini wametakiwa kujiunga na vikundi vya SACCOS ili kujijengea uzoefu wa ujasiriamali na uzalishaji. https://youtu.be/4DxyEvAJLZ8

SIMU.TV: Wakulima wadogo wa zao la mpunga kutoka wilaya ya Momba wameanza kupatiwa mafunzo ili waweze kujifunza namna bora ya uzalishaji wa zao hilo na kuinua vipato vyao.https://youtu.be/IwbCMgvuMi0

SIMU.TV: Michuano ya mpira wa kikapu ya Nyerere imeingia siku ya tatu ambapo timu shiriki za michuano hiyo zimeonekana kuwa na viwango bora. https://youtu.be/439ML0obOs0

SIMU.TV: Shirikisho la soka nchini TFF limesema kuwa haliutambui mkataba wa kuikodisha klabu ya Yanga hadi hapo litakapoupata mkataba huo na kuujadili.https://youtu.be/lgbqYEQuZrM

SIMU.TV: Kampuni ya simu ya Vodacom yaendelea kuwahimiza watanzania kujitokeza kushiriki shindano la jiongeze na M Pawa ili kujinyakulia zawadi kabambe kwa kujiwekea akiba. https://youtu.be/AbDK5Bucnog

SIMU.TV: Bondia wa uzani mkubwa duniani Tyson Fury kutoka Uingereza anakabiliwa na tuhuma za kudanganya kuwa mgonjwa na kutakiwa kurejesha mkanda wa ubingwa kwa WBO.https://youtu.be/6MAR2wZ9hDE

No comments: