Tuesday, October 18, 2016

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI NCHI AONGOZA WATUMISHI WA WIZARA YAKE KUAGA MWILI WA MWANASHERIA, MAREHEMU YUSTA MSOKA, JIJINI DAR

 Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lilian Mapfa akiaga mwili wa Mwanasheria wa Wizara hiyo, marehemu, Yusta Msoka, ambaye alifariki wiki iliyopita na mwili wake ulizikwa Mbagala, jijini Dar es Salaam jana. Nyuma ya Mapfa, ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa Wizara hiyo, Jane Massawe. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba, Afisa Sheria wa Wizara hiyo, Berious Nyasebwa wakiaga mwili wa mwanasheria mwenzao wa Wizara hiyo, marehemu, Yusta Msoka, ambaye alifariki wiki iliyopita na mwili wake ulizikwa Mbagala, jijini Dar es Salaam jana. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya (kushoto), Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Lilian Mapfa (kushoto kwa Balozi), Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara hiyo, Marlin Komba wakiwa katika hali ya huzuni pamoja na waombolezaji wengine wakati wa kuaga mwili wa marehemu, Yusta Msoka, ambaye alifariki wiki iliyopita na mwili wake ulizikwa Mbagala, jijini Dar es Salaam jana.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE), tawi la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, William Mkombozi akisoma wasifu wa Afisa Sheria wa Wizara hiyo, marehemu, Yusta Msoka, ambaye alifariki wiki iliyopita na mwili wake ulizikwa Mbagala, jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba, akikabidhi rambirambi kwa niaba ya Ofisi ya Mwajiri wa Afisa Sheria, marehemu Yusta Msoka. Kushoto anayepokea rambirambi hiyo ni Mama wa marehemu huyo. Mtumishi huyo alifariki dunia wiki iliyopita na kuzikwa jijini Dar es Salaam jana. 

No comments: