Tuesday, October 4, 2016

MJUMBE WA WAZIRI MKUU UINGEREZA NA WIZARA YA NISHATI NA MADINI WAJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI



Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (kushoto) akizungumza wakati wa mkutano huo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James na katikati ni Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza, anayeshughulikia Biashara na Uwekezaji nchini, Lord Hollick.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (kulia) akizungumza wakati wa mkutano wa kujadili fursa za uwekezaji kwenye Sekta ya Nishati nchini hususan nishati jadidifu. Katikati ni Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza, anayeshughulikia Biashara na Uwekezaji kwa Tanzania, Lord Hollick. Kushoto ni Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke.
Wajumbe kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake wakifuatilia majadiliano ya fursa za uwekezaji na Ujumbe kutoka Serikali ya Uingereza. Kushoto ni Kamishna Msaidizi anayeshughulikia Umeme, Mhandisi Innocent Luoga akifuatiwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji- Uwekezaji kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Declan Mhaiki.
Wajumbe wa mkutano uliokuwa ukijadili fursa za uwekezaji katika Sekta ya Nishati nchini wakiendelea na mkutano husika ulioongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (katikati mbele). Upande wa kushoto ni Ujumbe kutoka Serikali ya Uingereza na kulia ni Wataalam kutoka Wizarani.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (kulia) akimsikiliza Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza, anayeshughulikia Biashara na Uwekezaji kwa Tanzania, Lord Hollick.
Ujumbe kutoka Serikali ya Uingereza ukiongozwa na Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza, anayeshughulikia Biashara na Uwekezaji nchini, Lord Hollick (kulia) aliyeambatana na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (wa pili kutoka kulia) wakijadiliana jambo.

No comments: