Saturday, October 1, 2016

BODI YA TAIFA YA WAHASIBU NA WAKAGUZI WA HESABU (NBAA) YAFANYA MAHAFALI YA 38.




Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Kulia, akiwahutubia wahitimu na jumuiya ya Bodi ya taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) (Hawako Pichani), wakati wa mahafali ya 38 ya Bodi hiyo, yaliyofanyika katika Kituo cha Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam, kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, Bw. Pius Maneno na Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu na Mafunzo wa Bodi hiyo, Bi. Anne Mbughuni.
Baadhi ya wahitimu wa taaluma ya juu ya uhasibu (CPA), wakiwa tayari kutunukiwa shahada zao na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, katika Mahafali ya 38 yaliyofanyika Katika kituo cha Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) kilichopo Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akimkabidhi cheti cha kufanya vizuri katika masomo ya taaluma ya juu ya uhasibu (CPA-T), Bi. Happiness Ngowi, wakati wa mahafali ya 38 ya Bodi hiyo yaliyofanyika Katika kituo cha Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), kilichopo Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akitangaza kuwatunuku vyeti wahitimu wa taaluma ya juu ya uhasibu (CPA-T) waliofanya vizuri katika masomo yao, wakati wa mahafali ya 38 ya NBAA, yaliyofanyika Katika kituo cha Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu, kilichopo Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Wahitimu waliofanya vizuri katika masomo ya NBAA, baada ya kupokea vyeti vya kutambua umahili wao katika masomo pamoja na kupewa zawadi za fedha taslimu zilizotolewa na wadhamini mbalimbali wa Bodi hiyo, wakati wa Mahafali ya 38 yaliyofanyika katika Kituo cha NBAA, kilichoko Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.
Baadhi ya wahitimu wa shahada ya Juu ya Taaluma ya uhasibu na ukaguzi wa Hesabu CPA-T, inayotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), wakila kiapo cha utii na uadilifu wakati wa mahafali ya 38 ya Bodi hiyo, yaliyofanyika katika kituo kilichoko Bunju, Nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, (aliyeketi nafasi ya saba kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Bodi pamoja na wadhamini wa tuzo mbalimbali zilizotolewa kwa wahitimu waliofanya vizuri katika masomo yao, tukio lililofanyika katika kituo cha NBAA, kilichoko Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA Prof. Isaya Jairo (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA Pius Maneno, wakiondoka kwenye viwanja vya mahafali baada ya kumaliza kuwatunuku vyeti na shahada mbalimbali wahitimu wa kozi mbalimbali za NBAA, katika eneo la Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (kushoto), akisalimiana na Msajili wa Hazina Bw. Laurance Mafuru, baada ya kumalizika kwa mahafali ya 38 ya Bodi ya taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu(NBAA), yaliyofanyika katika kituo cha Bodi hiyo, Nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.
(Picha zote na Wizara ya Fedha) 

No comments: