Thursday, October 6, 2016

BENKI YA NMB TAWI LA NELSON MANDELA MJINI MOSHI WAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

Wateja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi wakipata kifungua kinywa na wafanyakazi wa benki hiyo katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja Duniani.
Keki maalumu iliyoandaliwa na Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Mjini Moshi kwa ajili ya wateja wake ktika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja Duniani.
Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi Emmanuel Kishosha akizungumza wakati akiwakaribisha wateja wa benki hiyo katika kuadhimisha siku ya huduma kwa wateja Duniani.
Baadhi ya wateja wakimsikiliza kwa makini Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi,Emmanuel Kishosha (hayupo pichani ) wakati akielezea historia ya benki hiyo ilipotoka na wapi ilipo sasa.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi,Butamo Nuru Ndalahwa wakimsikiliza kwa makini Meneja wa Benki ya NMB ,Emmanuel Kishosha (hayupo pichani).
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Butamo Ndalahwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja alipoalikwa na Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi.
Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela,Emanuel Kishosha akipeana mkono na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Butamo Ndalahwa.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akizungumza wakati wa maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja yaliyofanyika katika Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiwaongoza viongozi wengine,wateja na wafanyakazi wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi kukata keki wakiadhimisha wiki ya huduma kwa wateja.
Wafanyakazi wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi wakimlisha keki Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki katika maadhimisho hayo.
Meneja wa Benki ya NMB ,Emanuel Kishosha akimlisha keki Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Butamo Ndalahwa.
Wafanyakazi wa Benki ya NMB Moshi wakimlisha keki mfanyabiashara Patrick Boisafi kwa niaba ya wateja wa benki hiyo.
Mfanyabiashara Patrick Boisafi akimlisha keki Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi,Emanuel Kishosha.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiwa katika picha ya pamoja na wateja wengine wa benki hiyo pamoja na wafanyakazi wakati wa kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja Duniani.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: