Thursday, September 8, 2016

Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo yakutana na Wajumbe kutoka WADIGLA Misri

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Alex Nkenyenge(katikati) akionyesha mchoro wa mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Taifa na Uwanja wa Uhuru kwa Rais na Mwanzilishi wa WADIDEGLA kutoka Misri Bw. Adel Samy leo Jijini Dar es Salaam,kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa WADIDEGLA upande wa Afrika Bw.Rami Nashed. 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi. Joyce Hagu (wa kwanza kulia) akitoa maelekezo ya mchoro wa mradi wa kituo cha utamaduni kwa Rais na Mwanzilishi wa WADIDEGLA kutoka Misri Bw. Adel Samy leo Jijini Dar es Salaam. 
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Petro Lyatuu (kulia)akieleza jambo kwa Rais na Mwanzilishi wa WADIDEGLA kutoka Misri Bw. Adel Samy (kushoto), baada ya kikao kilichojadili masuala mbalimbali ya namna ya kuwezesha ushirikiano wa kuendeleza sekta zilizo chini ya wizara leo Jijini Dar es Salaam. 


Wajumbe wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo pamoja na wajumbe kutoka WADIGLA Misri wakifuatilia kwa makini fursa video iliyokuwa ikionyesha fursa mbalimbali zinazotolewa na WADIDEGLA Misri ikiwemo fursa katika sekta ya Michezo yenye lengo la kukuza na kuendeleza michezo mbalimbali. 




Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Petro Lyatuu akifafanua jambo wakati wa kikao na wajumbe kutoka WADIGLA Misri(hawapo katika picha), katika kujadiliana masuala mbalimbali na namna ya kuwezesha ushirikiano wa kuendeleza sekta zilizo chini ya wizara. 
Rais na Mwanzilishi wa WADIDEGLA kutoka Misri Bw. Adel Samy akieleza jambo wakati wa kikao na wajumbe kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo kilichokuwa kikijadili masuala mbalimbali ya namna ya kuwezesha ushirikiano wa kuendeleza sekta ya Michezo, leo Jijini Dar es Salaam,kulia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano kutoka Kampuni ya Montange Bibi. Teddy Mapunda 
Wajumbe wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo pamoja na wajumbe kutoka WADIGLA Misri wakifuatilia kwa makini fursa video iliyokuwa ikionyesha fursa mbalimbali zinazotolewa na WADIDEGLA Misri ikiwemo fursa katika sekta ya Michezo yenye lengo la kukuza na kuendeleza michezo mbalimbali.
Wajumbe wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo pamoja na wajumbe kutoka WADIGLA Misri wakifuatilia kwa makini fursa video iliyokuwa ikionyesha fursa mbalimbali zinazotolewa na WADIDEGLA Misri ikiwemo fursa katika sekta ya Michezo yenye lengo la kukuza na kuendeleza michezo mbalimbali. 
Picha na Lorietha Laurence-WHUSM.(08/09/2016).

No comments: