Thursday, September 29, 2016

Muhimbili Yaendesha Semina ya Kuimarisha Utoaji Huduma.

 Mtoa Mada, Martha Mkony akizungumzia vifo vya watoto na jinsi ya kutoa huduma bora kwa watoto wanaozaliwa kabla ya muda na njia ya kuzuia vifo kwa watoto hao.
 Baadhi ya washiriki wakisikiliza mada hiyo Leo katika hospitali hiyo.
 Dk Arvinder Singh akizungumzia umuhimu wa kununua vifaa tiba, kuwapo kwa madaktari na wauguzi wa kutosha, kuwapo kwa gesi ya uhakika, chumba cha kisasa cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu na madaktari na wauguzi kutoa huduma kwa wakati kwa watoto hao.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakiwamo madaktari na wauguzi wakifuatilia mada kwenye semina hiyo.
 Dk Hassan Mtani akitoa mada kuhusu kifafa cha mimba katika mkutano uliofanyika Leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). 
Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)

No comments: