Thursday, September 22, 2016

Benki ya Barclays yazindua program ya kuwawezesha wahitimu wa vyuo vikuu

 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Barclays Tanzania, Abdi Mohamed
(kushoto), akizungumza jijini Dar es Salaam leo, wakati wa uzinduzi wa
proram ya ReadytoWork inayolenga kuwapa elimu wanafunzi wa elimu ya
juu kujiandaa na ajira au kujiajiri. Wa tatu kushoto ni Mkuu wa Elimu
ya Juu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Lazaro Malili.
 Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Barclays Tanzania, Aron
Luhanga (kushoto), akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa
uzinduzi wa proram ya ReadytoWork inayolenga kuwapa elimu wanafunzi wa
elimu ya juu kujiandaa na ajira au kujiajiri. Kushoto kwake ni
Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Abdi Mohamed, Mkuu wa Elimu ya Juu,
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Lazaro Malili na Mkurugenzi
Mtendaji wa Shirika la Junior Achievement, Hamisi Kasongo.
 Mmoja wa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Kilonzo
Mringo (kushoto), akiuliza swali wakati wa uzinduzi wa proram ya
ReadytoWork ya Benki ya Barclays inayolenga kuwapa elimu wanafunzi wa
elimu ya juu kujiandaa na ajira au kujiajiri uliofanyika jijini Dar es
Salaam leo.

 Mkuu wa Elimu ya Juu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,
Lazaro Malili (kushoto), akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa
program ya ReadytoWork ya Benki ya Barclays inayolenga kuwapa elimu
wanafunzi wa elimu ya juu kujiandaa na ajira au kujiajiri uliofanyika
jijini Dar es Salaam leo.
Wasanii wa kikundi cha Mama Afrika wakitoa burudani wakati wa
uzinduzi wa proram ya ReadytoWork ya Benki ya Barclays inayolenga
kuwapa elimu wanafunzi wa elimu ya juu kujiandaa na ajira au kujiajiri
uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.

No comments: