Saturday, September 3, 2016

BALOZI WILSON MASILINGI AWASILI DURHAM, NC AFANYA MAZUNGUMUZO NA MAYOR

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Watanzania North Carolina (UTNC) Bi. Gloria Alex akimpokea na kukaribisha North Carolina Balozi wa Jamhuri wa Muungano ya Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi siku ya Ujumaa Septemba 2, 2016 City Hall mjini Durham, Northa Carolina katika ofisi ya Mayor ambapo Mhe. Balozi alikwenda kukutana na kufanya mazungumuzo na Mayor wa mji wa Durham Mayor William V." Bill Bell" (hayupo pichani,
Kushoto ni Mayor William V" Bill Bell" Mayor wa mji wa Durham akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi ofisini kwake siku ya Alhamisi Septemba 3, 2016 Mhe, Balozi alipokwenda kumtembelea na kufanyanae mazungumuzo.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akifanya mazungumuzo na Mayor wa mji wa Durham Mayor William"Bill Bell"
Mazungumuzo yakiendelea wengine katika mazungumuzo hayo kutoka kushoto kwa mzunguko wa meza ni Afisa Uhamiaji wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Bwn. Abbas Missana, Brady Surles ambaye ni Mkurugenzi mtendaji wa Sister Cities ya Durham yenye mashirikiano na mji wa Arusha, Tony Nturu, Dorothy Borden ambaye ndie mwanzilishi wa Sister Cities na Mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Gloria Alex,
Mazungumuzo yakiendelea.
Mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania North Carolina akiongea na Mayor William V"Bill Bell" na kumkaribisha kwenye mkutano wa Mhe. Balozi Wilson Masilingi atakapokutana na Watanzania wa Nortrha Carolina utakaofanyika leo Jumamosi Septemba 3, 2016 katika hotel ya Comfort Suites RDU iliyopo 5219 Page Road, Durham, NC 27703 kuanzia saa 12 jioni kwa saa za Marekani Mashariki(ET)
Mayor William V" Bill Bell" na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi katika picha ya pamoja.

Na mwandishi wetu, Durham, NC

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi siku ya Ijumaa Septemba 2, 2016 alimtembelea na kufanya mazungumuzo na Mayor wa mji wa Durham, North Carolina, Mayor William V. "Bill Bell".

Katika mazungumuzo hayo yaliyofanyika ofisi ya Mayor iliyopo City Hall, Mhe. Balozi Wilson Masilingi alimweleza Mayor William "Bill Bell" nia yake ya kutafuta wawekezaji watakaosaidia kukuza uchumi wa Tanzania kupitia seka mbalimbali huku akimweleza juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Magufuli za kufufua na kujenga viwanda,

Mhe. Balozi Wilson Masilingi alimhakikishia Mayor William "Bill Bell" wawekezaji watakaokua tayari kuwekeza Tanzania watafanyia taratibu zote na kwa haraka zaidi na bila kuwa na usumbufu huku Mayor William "Bill Bell" akimuahidi Mhe. Balozi William Masilingi kutoa ushirikiano wa karibu na kuhakikisha anamkutanisha na wawekezaji wa Durham, North Carolina watakaokua tayari kuwekeza nchini Tanzania.

No comments: