Thursday, August 11, 2016

vipaji Airtel Rising Stars vyamvutia RC Makalla, jijini Mbeya


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala amefungua rasmi mashindano ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars mkoa wa Mbeya na kuvitaka vilabu vya soka kutumia vipaji vinavyoibuliwa na programu hiyo ya vijana. Ufunguzi huo ulifanyika kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya leo Agosti 9, 2016.

“Hii ndio njia pekee ambayo inaweza kutuletea maendeelo ya soka na kuiwezesha nchi yetu kuondokana na matokeo mabaya katika mashindano mbali mbali ya kimataifa”, alisema. Aliishukuru kampuni ya Airtel Tanzania kwa kubuni programu hii ambayo imekuwa ikiwapa vijana fursa ya kuonyesha na kuviendeleza vipaji vyao.

Makala amewataka vijana kucheza kwa kujituma na kufahamu kwamba hatma ya mchezo wa soka hapa nchini iko mikononi mwao. Alilitaka Shirikisho la soka nchini (TFF) kufanya kazi kwa karibu na wadau wengine ili kuhakikisha kuwa vijana wanaoibuliwa kupitia Airtel Rising Stars wanaendelezwa.

Amewataka viongozi wa chama cha soka mkoa wa Mbeya (MREFA) kuyatumia vizuri mashindano ya Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa na kuchagua vijana nyota watakaounda timu za mkoa kushiriki kwenye fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zinazotarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Septemba 6 hadi 11 jijini Dar es Salaam.

Michuano ya Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa inaendelea katika mikoa minginge ambapo timu za wavulana za Makongo Sekondari na Kawe United zilitoshana nguvu baada ya kutoka suluhu katika uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam.

Fainali za Taifa zitashirikisha timu za wavulana na wasichana kutoka mikoa ya kisoka ya Ilala, Temeke na Kinondoni. Timu nyingine zitatoka Morogoro, Mwanza, Mbeya, Arusha, Lindi na Zanzibar.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Amoss Makalla aliye simama akizungumza na wachezaji kabla ya kuzindua michuano ya Airtel Rising Star kwa Mkoa wa Mbeya iliyo anza kutumia vumba jana katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na kushirikisha timu sita.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akisalimiana na wachezaji wa timu ya Dable 'A' ya jijini Mbeya kabla ya kuzindua rasmi michuano ya Airtel Rising Star Mkoa wa Mbeya iliyoanza jana katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya kwa kushirika timu sita za vijana.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla,akisalimia na mchezaji Alvira Zaibu wa tatu kushoto, kutoka timu ya soka ya watoto ya Mbeya Talent wakati wa ufunguzi wa Michuano ya Airtel Rising Star iliyonza kutimua vumbi jana katika dimba la Sokoine kwa kushirikisha timu sita za Mkoa Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akipiga mpira golkini ishara ya ufgunguzi rasmi ya michano ya mpira wa miguu kwa vijana chini miaka 17 Airtel Rising Stara iliyonza jana katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akifatalia mchezo wa ufunguzi wa michuano ya vijana chini ya miaka 17 Airtel Risin Star kati ya Mbaspo Academy dhidi ya Dable A zote kutoka jijini Mbeya uliomazika kwa Mbaspo kuibka na ushindi wa bao 4-0 ndani ya Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mbeya wakati wa uzinduzi wa michuano ya Airtel Rising Stars mkoani hapo
Wachezaji kutoka timu sita zinazo shiriki Michuano ya Airtel Rising Star chini ya miaka 17 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amsos Makalla hayupo katika picha kabla ya kuzindua rasmi michuano hiyo kimkoa jana katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

No comments: