Tuesday, August 23, 2016

Petro Itozya Magoti ahudhuria mafunzo ya uongozi nchini ujerumani, azungumza na billionea Knoop

Na Mwandishi wetu, Berlin 
Nilipata kusoma habari moja kutoka katika moja ya Vitabu vya Mwalimu Nyerere kuwa, Kijana anayetumia pesa na Chakula cha Kijiji,akitumwa ughaibuni kutafuta kilicho chema,kisha akapotelea huko asirejeshe chochote Nyumbani kwao,huyo atakua amefanya Uhaini.
Tunataka Vijana wanaokwenda Ughaibuni na kuleta Chakula Nyumbani.
Nimelazimika kuyakumbuka maneno haya baada ya kuona na kuskia habari za Petro Itozya Magoti (pichani),Kijana wa Kitanzania aliyeko Ulaya (hususani ktk Nchi ya Ujerumani) akihudhuria Mafunzo ya Uongozi na Mahusiano ya Siasa za Kimataifa.
Petro Magoti amepata fursa ya kipekee ya kuwa Mwakilishi wa Tanzania ktk Mafunzo hayo yanayohusisha Nchi 27 DUNIANI na ktk Bara la Afrika  wametoka Vijana 14 pekee na kati ya hao Tanzania wamechaguliwa Vijana 2, kwa bahati mbaya kijana mmoja hakuweza kuhudhuria kutokana na Majukumu aliyo nayo kwa sasa. Mafunzo hayo ni ya siku 60,tangu Augst 4, hadi Octoba 4 mwaka huu.

Msingi mkubwa wa Mafunzo hayo ni kuwaandaa Vijana katika Misingi ya Uongozi,pamoja na kujadili namna ya kutumia Fursa zilizopo ktk Nchi husika ili kuwawezesha zaidi kujiendeleza ktk Mahusiano ya Kitaifa na Kimataifa,kuwa na uwezo mahsusi wa kuzitumia Fursa zilizopo kwa Maendeleo ya Nchi zao.
Imepangwa mafunzo hayo yafanyike ktk Majiji Makubwa manne Nchini Ujerumani ambayo ni Berlin City, Humburge, Hannover na Munster, kisha Uholanzi ktk Majuma mawili ya Mwisho.
Hii ni Fursa ya kipekee kabisa kwa Vijana wa Afrika na hasahasa Tanzania kwani kupitia nafasi hiyo,licha ya kujifunza zaidi, Tanzania tutakua Mwakilishi wa kuitangaza Nchi yetu katika maswala ya Uchumi, Siasa na maswala ya Kijamii.
Kupitia Utangamano huo(Intergration) Tanzania inajipambanua zaidi katika Fursa zake za Kibiashara na Kitalii. Hivyo ni Matarajio yetu kuwa baada ya ukamilifu wa Mafunzo hayo kutafuatiwa faida kubwa zaidi za kiuchumi ktk Nchi yetu kutokana na uwekezaji.

PETRO MAGOTI AKUTANA NA KUFANYA 
MAZUNGUMZO NA BILLIONEA KNOOP. 
Katika kutekeleza adhima ya Serikali ya awamu ya Tano ya kuifikisha Nchi katika Mapinduzi ya Viwanda Vikubwa na Vidogo, Bwana Petro Magoti Mwakilishi pekee ktk Mafunzo hayo Nchini Ujerumani amekutana na mmoja wa Wamiliki wakubwa wa Viwanda Vikubwa Duniani Prof. KARL HEINZ KNOOP. Prof. Knoop anamiliki Viwanda ktk Nchi 17 Bara la Ulaya na Nchi 4 Barani Afrika.
Katika Mazungumzo yao,Prof. Knoop ambaye tayari ameonesha dhamira ya kuwekeza Nchini Tanzania ktk Maeneo ya Himo huko Moshi pamoja na Kilindi-Tanga, amebainisha dhamira yake ya kweli katika kuisaidia Serikali katika mpango wake huo wa Kuifikisha Nchi ktk Viwanda ili kutatua Tatizo la Ajira kwa Vijana Tanzania.
Hata hivyo, Prof. Karl Heinz Knoop ameeleza kuwa katika kutekeleza adhma yake hiyo kwa wakati,amekutana na Changamoto lukuki katika ukubalifu wa kupewa Eneo la Kujenga Viwanda Vikubwa vya Mashine za Kilimo kama vile Tractor, Mashine za Kupanda, Kuvuna na kukausha mazao ya Shamba pamoja na Maghala makubwa ya kuhifadhia Chakula.
Aidha, Prof. Knoop pia ameeleza dhamira yake ya kutaka kujenga Kiwanda cha Kutengeneza Magari Makubwa ya Mizigo(Semi-Tralers) Nchini Tanzania. Akifafanua zaidi, Prof. Knoop ameeleza kuwa Nje ya Changamoto hiyo ya kupatiwa Eneo, alikusudia kufanya utekelezaji wa mpango wake huo mapema kadiri itakavyowezekana ili kwenda sambamba na kasi ya Maendeleo ya Serikali ya awamu ya tano.

Katika Maelezo yake kwa Prof. Knoop, Bwana Petro Magoti, amemsihi na kumwomba Billionea Knoop kutokata tamaa ktk dhamira yake hiyo ya kujenga Viwanda Tanzania kutokana Changamoto ya kupata Eneo la Uwekezaji huo badala yake amemwomba kufika Tanzania ili Kuonana na Mh. Rais ambaye kwake Viwanda ni kipaumbele kikubwa. Bwana Magoti amemweleza kuwa,Mh. Rais wa Tanzania anavutiwa zaidi na wawekezaji walio tayari Kuijenga Tanzania ya Viwanda ili kukuza Uchumi wake na kupunguza tatizo la Ajira hasa kwa Vijana ambalo sasa ni kubwa zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali. Katika mapendekezo yake, Bwana Magoti amemshauli pia Billionea Karl Knoop kujenga Viwanda vyake ktk Mikoa ya Iringa na Morogoro ambayo ina maeneo mazuri kwa Kilimo.
Baada ya mazungumzo ya muda,Billionea Karl Heinz Knoop na Bwana Petro Magoti wamekubaliana kuwa kati ya tarehe 17 hadi 22 OCTOBEE,2016.Prof. Knoop atafika Tanzania kwa ajili ya kuonana na Mh. Rais ili kujadiliana nae juu ya Uwekezaji huo wa Viwanda na zana za Kilimo. Pia Knoop ameahidi kutembelea Mikoa ya Iringa na Morogoro ili kujiridhisha na maeneo hayo kwa ajili ya Uwekezaji ktk Viwanda vya Kilimo. 
Katika hatua nyingine ya kuhakikisha kuwa fursa hiyo inatumika ipasavyo, Bwana Magoti amepata nafasi ya kukutana na Wabunge Wastaafu na Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Ujerumani wakiongozwa na Prof. Hemker anaetokana na Chama cha SPD pamoja na Wazee walioshiriki ktk Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Katika Mazungumzo yao, Viongozi hao kutoka Kada mbalimbali Nchini Ujerumani wamekubali na kuahidi kuwa wako tayari kushirikiana na Rais wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli Kujenga Viwanda Vingi kadiri watakavyopata Fursa na nafasi ya kufanya hivyo. 
Katika kutekeleza dhamira hiyo wameahidi kujikita katika kujenga Viwanda vya Kutengeneza Mashine za Kupanda,kuvuna,kukausha Chakula,kuzalisha Mashine za kupukuchua Mahindi na nafaka Mbalimbali pamoja na Maghara ya kuhifadhia Chakula. Kwa kufanya hivyo watakua wametoa ajira nyingi kwa Watanzania ambao kilimo ni sehemu kubwa ya Maisha yao. 
Mafunzo ya Uongozi na Mahusiano ya Siasa za Kimataifa yanaendelea hapa Ujerumani kwa Wiki ya pili sasa. 
Tunaamini kuwa yapo Mengi ambayo Mwakilishi pekee wa Tanzania atajifunza kwa faida ya Nchi yetu. Lakini pia kutokana na jitihada zake, Tanzania itatambulika zaidi na kujipambanua juu ya Fursa zilizopo Nchini kwetu na kuwavutia zaidi Wawekezaji hasa ktk Sekta ya Kilimo na Viwanda. Ni katika hali hii ndio hasa Uchumi wa Nchi yetu unaweza kufikia kuwa wa kati katika miaka hii Mitano ijayo.
Ni maombi yetu Watanzania kwa pamoja kuwa Mungu awaongoze Watanzania wote wanaopata nafasi ya kuiwakilisha Nchi ktk Mataifa mbalimbali ili kuitambulisha Nchi yetu na fursa zake ktk uso wa Dunia kwa faida ya Watanzania wote.

Nchi yetu itajengwa na wenye Moyo.
Mungu awabariki sana!
#Berlin-Germany.

No comments: