Friday, August 26, 2016

mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania watembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohammed Janabi akizungumza na mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania. Kulia ni Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania, Edzai Chimonyo. Mabalozi hao wameitembelea taasisi hiyo ili kuona shughuli mbalimbali za kitibabu na wamehahidi kuwenda kupatiwa matibabu kwenye taasisi hiyo badala kwenda nchi nyingine ikiwamo Afrika Kusini kupatiwa huduma za magonjwa ya moyo.
Mabalozi wa nchi za Afrika nchini Tanzania wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohammed Janabi baada ya kuitembelea taasisi hiyo LEO.
Profesa Janabi akizungumza na mabalozi katika taasisi hiyo LEO.
Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano na mabalozi kwenye taasisi hiyo LEO.
Mabalozi hao wakiwa katika chumba cha upasuaji.
Mabalozi hao wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo. Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)

No comments: