Thursday, August 25, 2016

MAABARA ZA GST, TIRDO ZATEULIWA KUTHIBITISHA UBORA WA MAKAA YA MAWE

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akifafanua jambo katika mkutano na wachimbaji pamoja na watumiaji wa makaa ya mawe (hawapo pichani) uliojadili changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo. Mkutano huo ulifanyika Agosti 24, mwaka huu, Makao Makuu ya Wizara, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe, akizungumza na wachimbaji pamoja na watumiaji wa makaa ya mawe (hawapo pichani), wakati wa Mkutano baina yao na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani).  Mkutano huo ulifanyika hivi karibuni, Makao Makuu ya Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (kushoto kwa Waziri), wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yakiendelea wakati wa Mkutano baina ya Wizara na wachimbaji pamoja na watumiaji wa makaa ya mawe, uliofanyika Agosti 24 wizarani, jijini Dar es Salaam.

Wajumbe mbalimbali walioshiriki Mkutano baina ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Wachimbaji pamoja na Watumiaji wa Makaa ya Mawe, wakifuatilia mijadala mbalimbali katika Mkutano huo uliofanyika Agosti 24 mwaka huu Makao Makuu ya Wizara jijini Dar es Salaam.

No comments: