Wednesday, August 31, 2016

GEL YASAFIRISHA WANAFUNZI 70 VYUO VIKUU NCHINI INDIA



Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel, akizungumza na waandishi habari mjini Zanzibar juu ya safari wanafunzi 70 wanaokwenda kusoma nchini India.
Wanafunzi wakiingia katika feri ya Zanzibar kwa ajili ya safari ya kwenda vyu vikuu vya nchini India kupitia uwanja wa ndege wa zanzibar jana mjini Zanzibar
Wanafunzi wakipata historia katika makumbusho ya soko la watumwa wakati wa ukoloni ambalo lilifanyika Zanzibar.
Wanafunzi wakiingia katika basi kwa safari ya uwanja wa ndege wa Zanziabar kwa safari ya kwenda kusoma katika vyuo vya nchini India.
Wanafunzi wakiwa katika sehemu ya mapokezi ya uwanja wa ndege wa Zanzibar kwa ajili ya kuanza safari jana mjini Zanzibar.
Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel (Mwenye Bag) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi na baadhi ya wazazi waliowasindikiza watoto kwa ajili safari ya nchini India Jana Mjini Zanzibar
Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel (Mwenye Bag) akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa GEL katika uwanja wa Zanzibar.
Wanafunzi wakiingia katika boti ya kwenda Zanzibar kwa kwenda kusafiri kwa ndege kwa kutumia uwanja wa ndege wa Zanzibar.


MKURUGENZI wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel amesema kuwa kati ya 10 Wazazibar saba wanajua vyuo vya nje na tofauti ya Tanzania Bara hivyo kunahitajika kuwepo kwa ofisi ya kuratibu wanafunzi wanaotaka kusoma vyuo vya nje.

Mollel ameyasema mjini Zanzibar wakati alipokuwa anasafirisha wanafunzi 70 kwenda vyuo vya India kwa kupitia uwanja wa ndege wa Zanzibar, amesema kuwa kati ya sehemu ya kuongeza ofisi ni Zanzibar,Mwanza pamoja na Dodoma kutokana na serikal kuhamia huko .

Mollel amesema kupitia Zanzibar ni pamoja na kutaka wanafunzi hao wajue historia ya Zanziba katika makumbusho yalipokuwa Soko la watumwa ili wakifika huko waweze kuitangaza Tanzania uwepo wa vivutio hivyo.
Amesema wazazi wanatakiwa kufuata utaratibu uliowekwa na serikali na kuacha kutumia mawakala kwa kupeleka wanafunzi wanaokosa vigezo na mwisho wa siku wanakuwa hawana chakufanya nje na kuwa wazurulaji na kuipa doa nchi.

Aidha Mollel ameshauri wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi ambao hawana sifa ofisi za balozi ziwanyime viza katika kuleta heshima ya nchi kuwa watu wanaosoma nje ya nchi wanasifa za kujitosheleza na si vinginvyo.

Mollel amesema kuwa wanafunzi wanaopita GEL wanafuata taratibu zote ikiwa na vyuo wanavyokwenda vinatambulika ndani pamoja na bodi za nchi husika.Hata hivyo amesema wanafunzi wanaondoka vyuo vya nje vimeshafunguliwa tofauti ndani hivyo nafasi bado zipo kwa ajili wanafunzi wanaotaka kutimiza ndoto zao.

Mollel amesema ada ya vyuo vya nje na vyuo binafsi vya ndani ni sawa hivyo wazazi waache kuogopa hilo kutokana na mfumo uliowekwa baina ya Global Education Link na vyuo vya nje mzazi anaweza kulipa kwa awamu.

No comments: