Monday, July 18, 2016

WATANZANIA WAENDELEA KUTOA USHUHUDA JINSI PROMOSHENI YA TUSKER ILIVYOBADILI MAISHA YAO


Mmoja wa washindi wa Tusker milionea Albert Tarimo (kulia) akijadiliana jambo na fundi wa matofali Emmanuel Mboya (kushoto) ambayo aliyonunua kwa kutumia Milioni moja aliyoipata kutoka promosheni Tusker .

Mmoja wa washindi wa Tusker milionea Albert Tarimo (kulia) akijadiliana jambo na fundi wa matofali Emmanuel Mboya (kushoto) ambayo aliyonunua kwa kutumia Milioni moja aliyoipata kutoka promosheni Tusker


Ikiwa imebaki wiki moja tu kukamilisha wiki kumi za promosheni ya Milioni 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini, mwishoni mwa wiki ilichezeshwa droo ya nane ya promosheni hiyo huku washindi wengine kumi kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini wakitangazwa kujishindia vitita vya shilingi Milioni moja kila mmoja. 
 

Hii inafanya idadi ya washindi kufikia 90 tangu promosheni hiyo ianze wiki tisa zilizopita. Droo hiyo iliyofanyika katika studio za ITV na kushuhudiwa na wakaguzi wa wahesabu na Maofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini kuhakikisha droo imechezeshwa kwa kufata taratibu na masharti elekezi yaliyowekwa.

Washindi wa droo ya 8 ya Tusker Fanya Kweli Uwini ni :- God Muingi na Yohana Shirima kutoka Morogoro, Boniface Masanja na Selestin Simon kutoka Mwanza, Evarist Simwita kutoka Kilimanjaro, Obwor Nyambade kutoka Arusha, Rose Moses, Juliana Petro, Innocent Kiwango na Ally Mkemi kutoka Dar es Salaam.

“Tayari tumeshatoa 90,000,000 kwa watanzania na watumiaji wa bia ya Tusker, ni Milioni kumi tu ndo imebaki kwaajili yako wewe mteja wetu ili kukamilisha Milioni 100 tulizokusudia kutoa kwa wateja wetu. Ni furaha kubwa kwetu kuona wateja wengi wakiendelea kuwa na shauku ya kushiriki lakini wasife moyokwani bado tutaendelea kuwapa zawadi kibao zikiwemo bia za bure. Je ni kina nani watatukamilishia kumi ya mwisho?” alieleza kwa msisitizo Meneja wa Bia ya Tusker Jasper Migambile

Pia aliongeza kuwa Kampuni ya Bia ya Serengeti bado ina vitu viruri zaidi vinakuja kwa wateja wake kwani kuelekea ukingoni mwa mwa promosheni ya Tusker Fanya Kweli Uwini ni maandalizi ya kitu kinginekizuri zaidi. “Kila wakati tunawaza mambo mazuri kwa wateja wetu siku zote make mkao wa kula.” Aliongeza Jasper.Alisisitiza kuwa watanzania kuendelea kushiriki katika wiki hii ya mwisho mara nyingi kadiri wawezavyo ili waweze kuwa na nafasi za kushinda zaidi.

Promosheni ya Tusker Fanya Kweli Uwili ipo katika mfumo wa kuwazawadia wateja na watumiaji wa bia ya Tusker yenye lengo la kubadilisha maisha ya wateja wa Tusker katika njia tofauti. Wiki chache zilizopita Albert Tarimo alishinda Tsh 1,00,000 ambayo aliitumia kununulia tofalikwaajili ya kujengea nyumba yake katika kiwanja alichokua nacho muda mrefu lakini hakuweza kukiendeleza. Albert ambaye ni meneja wa baa amekiri kuwa maisha yake yamebadilika kupitia promosheni hiyo.

“Niliposhinda Milioni moja, moja kwa moja niliwaza kufanya kitu ambacho kitakua kinamanufaa kwangu na familia yangu. Tayari nilikua na kijisehemu changu nikaona chamsingi ninunue matofali ili nianze ujenzi taratibu. Mwanzo sikujua wapi naweza pata pesa za kununulia vifaa vya ujenzi wala hata namna ya kuanza msingi wa nyumba, lakini leo Tusker imeniwezesha nimenunua tofali 1000 ntakazotumia kuanza ujenzi hivi karibuni.

‘Tusker Fanya Kweli Uwini’ ni promosheni iliyoanza takribani wiki nane zilizopita mikoa yote nchini. Wiki moja tu imesalia kukamilisha washindi 100 wa promosheni hiyo.

No comments: