Monday, July 25, 2016

WAFANYAKAZI WA CRBD, TAWI LA MLIMANI CITY WAFURAHI PAMOJA NA KUCHEZA MICHEZO MBALIMBALI UFUKWENI.

Wafanyakazi wa benki ya CRDB tawi la Mlimani City wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufika katika ufukwe wa Milenium Bagamoyo Mkoani Pwani mwishoni wa wiki, Wafanyakazi hao ikiwa ni utamaduni wao wa kila mwaka kutembelea sehemu mbalimbali kwaajili ya kufurahi pamoja, kujenga mahusiano mazuri wakati wa kazi pamoja na kunywa na kula pamoja.

Akizungumza na Globu ya Jamii, Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City, Allen Killango amesema kuwa  wameamua kupumzika pamoja, kula na kunjwa pamoja mwishoni mwa wiki kwaajili ya kujenga mahusiano mazuri wakati wa kazi ikiwa ni siku mhimu sana kwao ambayo hufanyika kila mwaka.

Katika Mapumziko hayo ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City walikuwa na michezo mbalimbali ambayo walishiriki kama Mpira wa Mikuu kwa wote, Kuvuta Kamba, kukimbia na ndimu kwenye vijiko, Mpira wa wavu(Voleball) na kukimbia na Magunia.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City wakiwasili katika ufukwe wa Mileniam Bagamoyo Mkoani Pwani.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City wakipasha kwaajili ya kuanza kucheza Mpia wa Miguu.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City  mashindano wa timu mili za wafanyakazi hao zilipoanza kufuana katika mchezo uliochezwa mchangani katika fukwe za Milenium Bagamoyo Mkoani Pwani mwishoni mwa wiki.
Mtanange wa Mchangani ukiendelea kati ya Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City.
Mpira kati pale.
Kabumbu mchangani likisongeshwa na Refa Meneja uhusiano wa wateja binafsi, Stephen Makundi(Kulia aliyesimama)
Mfanyakazi Mlimani City na Kipa akishangilia baada ya Mpira kupigwa juu baada ya kukosa gori la timu Pinzani.
Mcezo ukiendelea.
Wakishangilia ushindi.
Mhhhh mchezo wa mpira ukienda sawia...
Maandalizi ya Mchezo wa Kamba.
Mchezo wa Kamba ukiendelea kati ya timu A na B ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City.
Hapa ni Vuta ni kuvute.
Hapa ni Kuvuta tuuuuuu.....
Kazi Kweli kwelii iiiiii........
Maandalizi ya Mchezo wa Kukimbia huku umevaa gunia.
Hapa mwendo wa kukimbi huku wenginemwingine akiishiwa pozi la kukimbia na kugusa mchanga kwa viwiko vya mikono.
Wadada wakiwa tayari  kwa kukimbia na magunia.
Mashindano ya kukimbia na magunia yakiendelea.
Maandalizi ya Mchezo wa Kukimbia na mdimu kwenye kijiko.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City wakikimbia na ndimu kwenye kijiko na kijiko kikiwa mdomoni.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City wa Timu A na B wakicheza mcheo wa Mpira wa wavu katika Fukwe za Milenium Bagamoyo Mkoani Pwani.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City wakiwa katika picha ya Pmaja mara baada ya kuogelea na wengine kugusa maji ya bahari.
Mameneja wa Benki ya CRDB tawi la Mlimani City wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza michezo mbalimbali katika Fukwe ya Milenium Bagamoyo Mkoani Pwani.

No comments: