Sunday, July 3, 2016

PSPF YADHIHIRISHA NI MFUKO CHAGUO NAMBA MOJA, WENGI WAJIUNGA NA MPANGO WA PSS MAONYESHO YA SABASABA

 Julita N Mongi, mwanachama mpya wa PSPF kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari, PSS, akionyesha kitambulisho chake cha uanachama alichokabidhiwa dakika 5 tu baada ya kujaza fomu. Huduma hiyo inatolewa kwenye banda la PSPF lililoko jengo la Wizara ya Fedha kwenye maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa, viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam Julai 3, 2016. Wananchi wengi wamejitokeza kujiunga na Mfuko huo na kudhihirisha kuwa ni chaguo la wengi. (PICHA NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID)
 Julita akikabidhiwa kadi yake na Afisa Masoko wa PSPF, Magira Werema
 Mstaafu ambaye kwa sasa ni Mkulima wa Turian, Mzee Gabriel E. Kiogwe (84), akijaza za kujiunga na mpango wa PSS
 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, akimkabidhi kadi ya uanachama, Mwanachama mpya,  Mzee Gabriel E. Kiogwe (84) dakika 5 baada ya kujaza fomu za kujiunga
 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, akimpiga picha Mwanachama mpya Scola Malinga
 Njaidi akimkabidhi kadi Scola Malinga, baada ya kujiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari, PSS
 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi akiwapatia maelezo ya kina ya faida za kujiunga na uanachama kwenye Mfuko huo, wafanyakazi wa wizara ya Fedha, ambapo baada ya maelezo hayo walijiunga na kuwa wanachama kupitia mpangio wa uchangiaji wa hiari, PSS.
 Joyce Kakore, akijaza fomu za kujiunga na mpango huo
 Joyce Kakore, wa wizara ya Fedha, (kulia), akikabidhiwa kadi ya kujiunga na uanachama PSPF, kupitia mpango wa PSS. Anayemkabidhi ni Afisa Uhusiano Mwandamizi, wa Mfuko huo, Abdul Njaidi
 Afisa Matekelezo wa PSPF, Penzila Kaisi, (kulia), akimpatia maelezo Mwanachama wa Mfuko huo aliyefika kwenye banda la PSPF, ili kujua hali ya michango yake
 Afisa wa PSS wa PSPF, SophiaMbilikira, (kushoto), akimsikiliza mwanachama wa PSPF aliyetembelea banda la Mfuko huo
 Mwanachama mpya wa PSPF, kupitia PSS, Lillingani S. Juma akionyesha kadi yake
  Julita N Mongi akijaza fomu
 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, (kulia) na Afisa Uwekezaji wa Mfuko huo Hawa Kivina, (wapili kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na wanachama wapya wa Mfuko huo dakika chache baada ya kukabidhiwa kadi zao
 Afisa Masoko wa PSPF, Magire Werema, (kushoto), akimkabidhi kadi ya uanachama wa PSPF, mwanachama mpya, Grace M Malya
 Grace M Malya akiwa amembeba mtoto wake, akionyesha kadi yake ya uanachama baada ya kukabidhiwa
 Wananchi wa kila kada wakipatiwa maelezo na maafisa wa PSPF kwenye banda la Mfuko huo
Afia Uhusiano Mwandamizi, wa PSPF, Abdul Njaidi akimkabidhi kadi ya uanachama mwanachama mpya Catherine D Mhina
 Afisa uwekezaji wa PSPF, Hawa Kivina, (kushoto), akimpatia maelezo Mwanachama wa Mfuko huo, Meneja Mawasiliano, Mamlaka ya Udhibiti Makampuni ya Bima Tanzania, Eliezer Rweikiza, juu ya mikopo ya nyumba
Hadji Jamadari, Afisa Mwendeshaji Mkuu wa PSPF, akichapisha vitambulisho vya wanachama wapya papo hapo na kuwakabidhi
Catherine D Mhina, akionyesha kadi yake

No comments: