Thursday, July 28, 2016

MKUU WA WILAYA KISHAPU AFUNGUA MAFUNZO YA MGAMBO

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Ngabaganga Taraba akifungua mafunzo ya mgambo katika kata za Mwaweja na Ukenyenge wilayani humo, ambapo aliwataka vijana kuwa wazalendo. Akiwapongeza kwa kujitoa kwao kuhudhuria mafunzo hayo, alisema suala la ulinzi wa mali na raia ni la kila mwananchi. Aliwataka kutumia mafunzo hayo kwa mtazamo chanya na kuwa mabalozi wazuri wa amani na uzalendo kwa nchi yao. Aidha, Taraba aliwapongeza wakufunzi wa mafunzo hayo kwa kazi nzuri ya kuwafundisha vijana stadi za ukakamavu ili wawe walinzi wazuri wa amani.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kishapu, Shadrack Kengese akimkaribisha Mkuu wa Wilaya kuzungumza na vijana wanaopata mafunzo hayo pamoja na watendaji wa vijiji mbalimbali wa kata hizo waliofika viwanjani hapo. Wengine kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga, Mkuu wa Wilaya hiyo, Nyabaganga Taraba na kulia ni Afisa kutoka Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji, Yusuf Kambi.
Vijana wanaopitia mafunzo ya mgambo wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Ngabaganga Taraba wakati akitoa nasaha zake kwao alipofungua mafunzo hayo kata za Ukenyenge na Mwaweja wilayani humo.
Vijana wakipita kwa ukakamavu mbele ya Mkuu wa Wilaya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kishapu, Ngabaganga Taraba pamoja na viongozi mbalimbali walipoonesha namna wanavyopata mafunzo hayo kutoka kwa wakufunzi wao.
Sehemu ya wananchi na watendaji wa vijiji mbalimbali vya kata za Ukenyenge na Mwaweja wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kishapu wakati akizungumza alipofungua mafunzo ya mgambo wilayani humo. Kushoto ni Mshauri wa Mgambo Wilaya, Charles Lyambisha.
Sehemu ya wananchi na watendaji vijiji wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Kishapu, Ngabanga Taraba wakati akifungua mafunzo ya mgambo kata za Ukenyenge na Mwaweja.

No comments: