Sunday, July 10, 2016

Benki ya NBC yazindua Program ya Wajibika kusaidia ajira kwa vijana wanaohitimu vyuo na taasisi ya elimu ya juu

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Anthony Mavunde (wa pili kulia), na Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), James Kinyanyi (wa pili kushoto), wakibonyeza kitufe cha kompyuta kuashiria uzinduzi wa program ya Wajibika ya NBC yenye lengo la kuwandaa vijana wahitimu wa vyuo na taasisi za elimu ya juu kuingia soko la ajira rasmi na binafsi katika hafla iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia kushoto ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Utawala), Prof. Cuthbert Kimambo na Mkurugenzi wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Anthony Mavunde, akishiakana mikono na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC Tanzania, Neema Rose-Singo (kushoto), baada ya kuzindua program ya Wajibika ya NBC yenye lengo la kuwandaa vijana wahitimu wa vyuo na taasisi za elimu ya juu kuingia soko la ajira rasmi na binafsi katika hafla iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wapili kushoto ni; Meneja Mahusiano wa NBC, William Kallaghe, Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa NBC, James Kinyanyi, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Utawala), Prof. Cuthbert Kimambo na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu, James Kajugusi.
Mkurugenzi wa Bodi ya Benki ya NBC, Dk. Kassim Hussein (kulia), akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa program ya Wajibika ya benki hiyo yenye lengo la kuwandaa vijana wahitimu wa vyuo na taasisi za elimu ya juu kuingia soko la ajira rasmi na binafsi katika hafla iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wengine kutoka kushoto ni; Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa NBC,James Kinyanyi, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Utawala), Prof. Cuthbert Kimambo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Anthony Mavunde, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu, James Kajugusi na Meneja Mahusiano wa NBC, William Kallaghe.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Anthony Mavunde (kulia), akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa program ya Wajibika ya Benki ya NBC yenye lengo la kuwandaa vijana wahitimu wa vyuo na taasisi za elimu ya juu kuingia soko la ajira rasmi na binafsi katika hafla iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Meneja Mahusiano wa NBC, William Kallaghe akizungumza katika hafla hiyo katika Ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mlimani jijini Dar es Salaam juzi.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Anthony Mavunde (katikati), akiongozana na Meneja Mahusiano wa NBC, William Kallaghe(kushoto), na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Utawala), Prof. Cuthbert Kimambo (kulia), wakati akiingia katika Ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam juzi kuzindua program ya Wajibika ya Benki ya NBC yenye lengo la kuwandaa vijana wahitimu wa vyuo na taasisi za elimu ya juu kuingia soko la ajira rasmi na binafsi.
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi huo.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na washiriki wengine waliohudhuria uzinduzi huo wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa program ya Wajibika ya Benki ya NBC, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu, Anthony Mavunde (katikati),akipozi kwa picha ya kumbukumbu pamoja na maofisa wa NBC na wageni wengine mashuhuri.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa program ya Wajibika ya Benki ya NBC, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu, Anthony Mavunde (katikati),akipozi kwa picha ya kumbukumbu pamoja na maofisa wa NBC ambao kwa namna moja ama nyingine wamefanikisha uzinduzi huo.

No comments: