Tuesday, June 14, 2016

ZIARA YA SERIKALI YA JIMBO LA PUNTLAND-SOMALIA NCHINI TANZANIA


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro akifafanua jambo wakati wa kikao na ujumbe kutoka Serikali ya Jimbo la Puntland -Somalia walipoitembelea Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo. Kulia kwake ni Waziri wa Kazi, Vijana na Michezo wa Serikali ya Jimbo la Puntland – Somalia, Mhe. Abdirahman A. Abdulle.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro akiukaribisha ujumbe kutoka Serikali ya Jimbo la Puntland - Somalia, ulipoitembelea Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo. Kulia kwake ni Waziri wa Kazi, Vijana na Michezo wa Serikali ya Jimbo la Puntland – Somalia, Mhe. Abdirahman A. Abdulle akiwa na Maafisa alioambatana nao.
Waziri wa Kazi, Vijana na Michezo wa Serikali ya Jimbo la Puntland –Somalia, Mhe. Abdirahman A. Abdulle akizungumzia lengo la Serikali yake kuitembelea Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo. Kulia kwake ni Maafisa aliombatana nao.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Henry Mambo akieleza namna Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kitakavyoshirikiana na Serikali ya Jimbo la Puntland – Somalia katika kuijengea uwezo Sekta ya Umma ya Serikali hiyo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro akibadilishana kadi za mawasiliano na baadhi ya Maafisa kutoka Serikali ya Jimbo la Puntland - Somalia mara baada ya hafla fupi ya kuwakaribisha katika Ofisi ya Rais-Utumishi iliyofanyika mapema leo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Serikali ya Jimbo la Puntland -Somalia walipoitembelea Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.

No comments: