Friday, June 3, 2016

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA ATAKA RAIS DR MAGUFULI AOMBEWE.


Waziri wa kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba akizindua tamasha la urafiki katika viwanja vya Ndege mjini Morogoro jana Juni 2 ,tamasha lililoandaliwa na ushirikiano wa makanisa katika mkoa wa Morogoro na kuongozwa na mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt. Kabwe Steven Kabwe kulia na waziri wa Kilimo ,Mifugo na Uvuvi wakiwapungia wananchi wa Morogoro mikono wakati wakiwasili katika viwanja vya Ndege kwa ajili ya uzinduzi wa tamasha la Urafiki lililoanza jana Juni 2 hadi Jumapili Juni 5.
Waziri wa kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba ambae ni mbunge wa jimbo la Iramba akiwapungia mikono wananchi wa Morogoro wakati akiwasili katika viwanja vya Ndege kuzindua tamasha la Urafiki.
Mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren ambae anaongoza tamasha la Urafiki mjini Morogoro akimpongeza waziri wa Kilimo ,Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba baada ya kuwasili mkoani Morogoro kuzindua tamasha hilo.
Waziri Nchemba akimsikiliza mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren.
Mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akiwa katika picha ya pamoja na waziri wa kilimo ,Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba.
Waziri Nchemba akipokelewa na RC Morogoro Dkt. Kabwe Steven Kabwe .
Waziri Nchemba akiwasili uwanja wa mkutano.
Mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren wa pili kushoto akiwa na waziri wa kilimo ,Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba pamoja na viongozi waandaaji wa tamasha la Urafiki Morogoro kushoto wa kwanza ni Askofu wa kanisa la Philndelphia Dr Yohana Masingu.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt. Kabwe Steven Kabwe kulia akiwa na waziri Nchemba.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt. Kabwe Steven Kabwe kulia akimwongoza waziri Nchemba.
Mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akiteta jambo na waziri Nchemba 


Mapokezi ya waziri Nchemba Morogoro.








Kwaya ikitumbuiza katika uwanja huo.



Waziri Nchembe akizindua tamasha hilo.

Mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akiendelea kuhubiri 
Wananchi wakiwa katika viwanja hivyo.





Mtoto ambae alikuwa hasikii toka azaliwe akijaribiwa baada ya kuombewa na kupona.
Mwanamke aliyekuwa kapooza akitembea baada ya maombi.
Mmoja kati ya watu walioanguka kwa mapepo uwanjani wakati wa maombi.
Mkazi wa Morogoro aliyekuwa anatembea kwa shida baada ya kuotwa na uvimbe mkubwa eneo la siri akiruka ruka kwa furaha baada ya kuombewa na kupona na mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren.
Mwanamke ambae alikuwa na matatizo ya kusikia kwa miaka zaidi ya 15 akitoa ushuhuda baada ya kuombewa na mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren kushoto .
Mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akihubiri katika tamasha la Urafiki mjini Morogoro .
Na MatukiodaimaBlog, Morogoro.
WAZIRI wa Kilimo , Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba amelaani mauwaji ya kinyama kikatili yanayoendelea kuibuka nchini kuwa yasipewe nafasi na kutaka kila mtanzania kwa imani yake kuliombea Taifa kuondokana na mauwaji hayo pia wakati wote kutoacha kumwombea Rais Dr John Magufuli kwani kazi anayoifanya ni ngumu zaidi.

Huku akichangia Tsh milioni 2 ili kuchangia huduma za tamasha la Urafiki la kuliombea Taifa mkoani Morogoro kuendelea mjini Morogoro kwa madai kuwa huduma hiyo ni tiba ya maovu yanayoendelea kujitokeza hapa nchini kwa watu kuchinjwa kikatili kila kona ya nchini.

Waziri Nchemba alisema kuwa tukio la mashekhe na waumini wao kuchinjwa msikitini si jambo ambalo watanzania tumezoea kuliona ama kusikia pia mauwaji ya Mwanamke Aneth Msuya wa Dar es Salaam na watu nane kuchinjwa Tanga na lile la Mwanza si matukio ambayo yamezoeleka Tanzania , hivyo kutaka suala hili lisiachwe kuendelea na badala yake kuzidi kuliombea Taifa . 

“ Tunapokusanyika na tunapokuwa faragha katika ibada zetu tuliombee taifa letu ……jambo la pili kwa uzito huo huo tumwombee Rais wetu mpendwa Dr John Magufuli kazi anayoifanya ni ngumu … kazi anayoifanya ni kwa niaba ya watanzania wote na utashi ule anaoendanao ninyi wenyewe mliomba sana kabla ya kumpigia kura ….uzoefu unaonyesha mabadiliko huwa hayaji rahisi rahisi adui huwa hakubali kushindwa kirahisi kwa hiyo kila tunapoongea na Mungu wetu tukumbuke kumwombea Rais wetu ili kila mema anayoliwazia Taifa yaweze kutimia” alisema waziri Nchemba 

Kuwa kwa upande wake kila anapoona watumishi wa Mungu wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya huduma huwa haachi kuwasogelea japo kushikana nao mikono kama sehemu ya kupokea baraka kutoka kwao kwani wapakwa mafuta wakisema tu ubarikiwe Mungu juu mbinguni huweka tiki ya baraka. 

“Na hivyo ndivyo nilivyopata hata ubunge nilikuwa sina gari wala baiskeli na wazazi wangu walikuwa wanaishi katika nyumba ya tembe wakiwa na maisha magumu nikaenda kanisani kulikuwa na Harambee japo sikuwa na pesa nyingi niliamua kuchangia kidogo tu …..watumishi wale wakasema Ee Mungu mjalie haja ya moyo wake huyu kijana na mimi nilikuwa nikiwaza ubunge kweli ubunge ukatiki …..na hivi leo amekuja mhubiri wa kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren akasema kwa lugha ya kiingereza kuwa Ee Mungu timiza ndoto ya kijana huyo na mimi ndogo hiyo inaendelea kuota hivyo hivyo kwa hiyo najua na ninyi mtanikumbuka katika majukumu ambayo nimepewa na Rais ……leo baada ya saa 4 asubuhi hatukuwa na ratiba ya vikao vya bunge nimelazimika kuja Morogoro kuifanya kazi hii na leo hii nitageuza bungeni “ 

Kwani alisema majukumu ambayo anayatumikia pia yana harufu ile ile ya ambayo amewaomba kuzidisha maombi kuliombea Taifa kwani yana harufu ya umwagaji wa damu . 
Alisema waziri Nchemba kuwa alipoteuliwa na Rais Dr Magufuli kabla hata ya kuapishwa alipata taarifa ya mifugo kuuwawa na watu kuchinjana kwa kukatana mapanga mkoani Morogoro ambayo yalimkumbusha mapigano ya chuki na wivu kwa Abeli na Kaini mmoja akiwa mkulima na mwingine mfugaji.

“ Tuliombee Taifa letu kila mmoja afanye kazi inayomlete kipato pasipo kuwa na wivu na bila kuwa na dharau kwa kazi ya mwenzake ….kila nikipita huwa nawaeleza watumishi wangu kuwa hakuna mali ,mifugo,shamba ama kitu chochote chenye dhamani kubwa kuliko uhai wa mwa wanadamu” 

Kuwa serikali itatengeneza mazingira bora ya wakulima ama wafugaji kufanya kazi zao kwa uhuru na amani japo kila mmoja anapaswa kutambua kuwa uhai ni zaidi ya yote. 

Kwa upande wake mhubiri wa huyo kimataifa toka nchini Canada Dr Peter Youngren limpongeza waziri Nchemba kwa kujiweka mbele katika huduma&nbs ...

No comments: