Wednesday, June 8, 2016

VITUO VYA TAARIFA NA MAARIFA VYAPIGWA MSASA NA TGNP

 Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi Lilian Liundi akifungua semina  kwa Wanaharakati pamoja na viongozi wa vituo vya taarifa na Maarifa waliofika katika semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa TGNP Mtandao leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Geofrey Adroph)
Mkuu wa Program ya Taarifa na Utafiti kutoka TGNP, Gloria Shechambo akitoa elimu kwa wanaharakati kuhusu utendakazi wao wa kila siku wakati wa semini iliyofanyika katika ukumbi wa TGNP Mtandao.
 Katibu wa Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kata ya Kibuko, Bw. Valentino Lukoo akitoa ufafanuiz kuhusu maendelea yaliyofikia katika kata yao baada ya kuonekana kwa changamoto nyingi katika kata hiyo
 Mwenyekiti wa Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kata ya Igale, Bi Lidya Sankemwa Mwakalinga akizungumzia mipango ya kata yao kuhusu utoaji wa taarifa husika katika kata yao.
 Mwanaharakati kutoka Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kata ya Nsalal  Bi. Felister Kais akizungumzia changamoto wanazozipata katika utoaji wa taarifa.
Mwanaharakati kutoka  Mabibo, Bw. Furaha Mbakile akichangia mada
 Afisa program Utafiti na Uchambuzi kutoka TGNP, Bw. Alphonce Stima akiongea jambo wakati wa utoaji wa Semina kwa Wanaharakati pamoja na viongozi wa vituo vya taarifa na Maarifa waliofika katika semina hiyo

Wanaharakati pamoja na iongozi wa vituo vya taarifa na Maarifa wakitazama hotuba ya  Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango anasoma na kuwasilisha Hali ya Uchumi kwa mwaka 2015 na Mpango wa Maendeleo Bungeni 
 Afisa program Utafiti na Uchambuzi kutoka TGNP, Bw. Alphonce Stima akiongea jambo mara baada ya kumalizika kwa Hotuba  ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango anasoma ama kuwasilisha Hali ya Uchumi kwa mwaka 2015 na Mpango wa Maendeleo Bungeni Dodoma
Afisa Programu mwandamizi wa Ushawishi na utetezi kutoka TGNP Mtandao, Bi. Anna Sangai akitoa elimu wanaharakati pamoja na viongozi wa Taarifa na Maarifa katika ukumbi wa TGNP jijini Dar es Salaam leo
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake katika Jitihada za Maendeleo (WAJIKI), Janeth Mawinza akichangia mada
 Afisa Program uchambuzi na Machapisho kutoka TGNP Mtandao, Bw. Deogratius Temba akiwaeleza wanaharakati pamoja na viongozi wa Taarifa na Maarifa jinsi ya ufanyakazi wa TGNP Mtandao

Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi Lilian Liundi(kulia) akifuatilia Bunge kupitia njia ya Television katika ofisi ya TGNP  Mtandao



 Baadhi ya Wafanyakazi wa TGNP Mtandao, Wanaharakati, viongozi wa Taarifa na Maarifa pamoja na wananchi wakifuatilia Bunge kwa njia ya Televisioni ndani ya Ukumbi wa TGNP Mtandao jijini Dar es Salaam

No comments: