Wednesday, June 1, 2016

TAASISI YA BENJAMINI MKAPA NA THET WASAINI MKATABA KWAJILI YA MAFUNZO YA AFYA YA JAMII.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa (BMF), Ellen Mkondya-Senkoro akizungumza jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na Maendeleo ya Mradi wa miaka mitatu ambao utashirikisha vyou vya afya ya jamii pamoja na hospitali za rufaa za kanda ya ziwa pamoja na kusaini mkataba ya makubaliano ya kuendesha mradi wa wataalamu wa afya ya jamii pamoja na watu wa kada ya afya wa mikoa ya kanda ya ziwa. 

Amesema kuwa mradi huo unashirikisha Taasisi ya Benjamini Mkapa, Tropical Health Education Trust(THET) pamoja na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwaajili ya kuwapa mafunzo wafanyakazi pamoja na wafunzi wa vyuo kwaajili ya kuimarisha afya ya jamii hapa nchini.

Ellen amesema kuwa Mradi wa kada ya afya umeshaanza tangu Machi huu na utagharimu kiasi cha shilingi bilion 3.3 kwaajili ya kuimarisha uwezo wa Afya ya Jamii hapa nchini ambao unalenga katika kuimarisha vyuo vya Afya kumi na (Teaching Hospital) Mafunzo katika hospitali za kanda ya ziwa.

Vyuo hivyo vilivyopo mikoa ya kanda ya ziwa vya kada ya afya ni Bukumbi school of Nursing, Ngudu School of Invironmental Health, Tandabui Institute of HST, Geita Nursing & Midwifery School, Bishop Kisula College of HS, Rubya Health Training Institute, Karagwe Institute of Allied Health Sciencies, Murugwanza School of Nursing, Kahama SON, Kolandoto of Nursing na Hospitali za Rufaa za kanda ya ziwa zitakazo fikiwa na mradi huoni Sekou Toure Geita Regional Referral Hospital, Kagera na Shinyanga.
Kuanalia uhaba wa watumishi wa afya.
Meneja Mwakilishi Mkazi wa Tropical Health Education Trust(THET) Tanzania, Godwin Kabalika akizungumza jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na kusaini Mkataba wa kushirikiana katika kutoa mafunzo ya afya ya jamii ili kupunguza uhaba wa wafanyakazi wa kada ya afya hapa nchini.
amesema kuwa kupitia mradi huo wataalam wa afya ya jamii wataongezewa ujuzi pamoja na wanafunzi wa vyuo vya kanda ya ziwa watapata ujuzi ambao utakua unastahili. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa (BMF), Ellen Mkondya-Senkoro.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa (BMF), Ellen Mkondya-Senkoro (Kushoto) na Meneja Mwakilishi Mkazi wa Tropical Health Education Trust(THET) Tanzania, Godwin Kabalika (Kulia) wakisaini mkataba kati Taasisi ya Mkapa na Tropical Health Education Trust(THET) kwaajili ya kutoa mafunzo kwa wananchi wa kada ya Afya ya Jamii pamoja na wafanyakazi wa kada ya afya waliopo katika huspitali zilizopo hospitali za rufaa za kanda ya ziwa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Benjamini Mkapa (BMF), Ellen Mkondya-Senkoro (Kushoto) na Meneja Mwakilishi Mkazi wa Tropical Health Education Trust(THET) Tanzania, Godwin Kabalika (Kulia) wakibadilishana mikataba jijini Dar es Salaam leo, Kwaajili ya mradi ambao umaeshirikisha Taasisi pamoja na serikali kwaajili ya kusaidi wataalam pamoja na wanafunzi wa kada ya afya hapa nchini.

No comments: