Friday, June 24, 2016

TAA YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI KWA IDARA YAKE YA RASILIMALI WATU NA ILE YA BIASHARA KUKUTANA NA WANANCHI NA WATUMISHI.


Meneja Rasilimali Watu Mafunzo wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Abdul Mkwizu (kulia) akimpa maelezo kuhusu mafunzo Ally Zongo Mfanyakazi wa taasisi hiyo, kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2016.
(PICHA NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID).
 Afisa Rasilimali Watu Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Fatma Matimba, akifanya kazi ofisini kwake jijini Dar es Salaam, wakati wa kilele cha siku ya Utumishi wa Umma ambapo mwaka huu, maadhimisho hayo yamefanyika mahala pa kazi ambapo wananchi pamoja na wafanyakazi wa taasisi husika walipata fursa ya kujipatia elimu ya shughuli mbalimbali zifanywazo na taasisi husika.
Afisa Rasilimali Watu Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Fatma Matimba (kushoto) akitoa ufafanuzi juu ya upandishaji vyeo kwa wafanyakazi Omari Hazaa (katikati) na Yusuph Mahadhi (kulia), ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, 2016. 

No comments: