


Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Tulla Mwigune (kulia) Afisa Michango wa Mfuko huo, Saluna Aziz Ally (katikati) na Afisa Michango Glory Maboya, wakijiandaa kuhudumia wateja leo asubuhi katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba.


Afisa Uwekezaji wa Mfuko huo, Jonas Mbwambo akiweka mambo sawa kabla ya kuanza kupokea wateja katika Banda lao namba 86 viwanja vya Saba saba.

Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Pauline Msanga, akitoa maelezo kwa wananchi kuhusu Huduma za uendeshaji Mfuko huo, wakati walipotembelea katika Banda lao lililopo kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, leo.

Sehemu ya wananchi waliotembelea Banda la Mfuko wa Pensheni wa PPF wakipata elimu kuhusu Mafao yatolewayo na Mfuko huo na jinsi mwanachama anavyoweza kujiunga na kuchangia.

Afisa Michango wa Mfuko huo, Saluna Aziz Ally, akimfafanulia mwanachama wake kuhusu uchangiaji wa michango ya Wanachama,

Afisa Huduma kwa Wateja wa PPF, Mwajuma Msina, akizungumza na Mwananchi aliyefika kutembelea Banda hilo wakati akimwelezea kuhusu huduma zinazotolewa na Mfuko huo.

Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Tulla Mwigune (kulia) akifafanua jambo kwa mstaafu wa PPF.

Mtaalamu wa Mifumo ya Habari wa Mfuko wa PPF, Isabela Ngalawa, akimwelekeza mmoja kati ya Wanachama wa Mfuko huo kuhusu 'PPF Taarifa Mobile Apps' ili mwanachama aweze kupata taarifa za michango yake kupitia simu yake ya mkononi.

Afisa Huduma kwa Wateja, Mohamed Siaga, akizungumza na Mwananchi aliyefika katika Banda la PPF kuhusu jinsi ya kujiunga na Mfumo wa 'Wote scheme kutoka sekta isiyo rasmi.

Mmoja kati ya Wanasheria wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nyambilila Ndoboka, akimwelekeza jambo mwanachama wa Mfuko huo kuhusu masuala ya Kisheria, wakati alipofika kutembelea Banda la Maonesho la PFF leo.


Picha Zote na Mafoto Blog
No comments:
Post a Comment