Sunday, June 5, 2016

MABALOZI KENYA WAADHIMISHA SIKU YA AFRIKA

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Rodriguez  Alvaro (kulia) akizungumza na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (kulia) mara baada ya kufika Ofisini kwake Bungeni Dodoma leo.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (kulia) akizungumza na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini Tanzania , Rodriguez  Alvaro (kulia) mara baada ya mwakilishi huyo kufika Ofisini kwake Bungeni Dodoma leo.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Rodriguez  Alvaro (kulia) akimwonesha Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (kulia) sehemu ya taarifa ya mwaka ya utekelezaji wa programu mbalimbali za Umoja wa Mataifa nchini mara baada ya kufika Ofisini kwake Bungeni Dodoma leo.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Rodriguez  Alvaro (kulia) akimkabidhi Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (kulia) taarifa ya mwaka ya utekelezaji wa programu mbalimbali za Umoja wa Mataifa nchini mara baada ya kufika Ofisini kwake Bungeni Dodoma leo.
Wabunge Mhe. Margaret Sitta (Kushoto) na Mhe. Najma Murtaza Giga, Mwenyekiti wa Bunge wakiwa katika picha ya pamoja kwenye rangi za Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu 17 ya dunia wakati wa Semina ya wabunge kuhusu mchango wao katika utekelezaji wa malengo hayo nchini iliyofanyika Bungeni, Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini Tanzania , Rodriguez  Alvaro (kulia) kwenye rangi za Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu 17 ya dunia wakati wa Semina ya wabunge kuhusu mchango wao katika utekelezaji wa malengo hayo Bungeni Dodoma leo.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiwa ameshika mabango mawili yenye malengo mapya 2 ya Maendeleo Endelevu kati ya 17 ya Umoja wa Mataifa yanayotakiwa kutekelezwa duniani kote kuanzia mwaka huu hadi 2030.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (kushoto) katika picha ya pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini Tanzania , Rodriguez  Alvaro (kulia) wakiwa na mabango yenye Malengo Mapya 2 kati ya 17 ya dunia wakati wa Semina ya wabunge kuhusu mchango wao katika utekelezaji wa malengo hayo Bungeni Dodoma leo.
Mbunge wa Urambo Mhe. Margaret Sitta (Kushoto) na Mhe. Najma Murtaza Giga, Mwenyekiti wa Bunge wakiwa katika picha ya pamoja kwenye rangi za Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu 17 ya dunia wakati wa Semina ya wabunge kuhusu mchango wao katika utekelezaji wa malengo hayo nchini iliyofanyika Bungeni, Dodoma.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Rodriguez  Alvaro akizungumza na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Semina Kuhusu Malengo ya dunia iliyoandaliwa na Umoja huo mjini Dodoma leo.
 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akizungumza na Wabunge wakati wa ufungunzi wa Semina kwa wabunge kuhusu Malengo ya dunia iliyoandaliwa na Umoja huo mjini Dodoma leo.
Mabango yenye Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu 17 ya dunia.

Mtaalam wa Masuala ya Uchumi kutoka Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP), Rodgers Dhliwayo akiwasilisha mada kuhusu namna ya kuyafikia Malengo Mapya 17 ya dunia wakati wa Semina ya Wabunge kuhusu malengo hayo mjini Dodoma.
Mtaalam wa Masuala ya Uchumi kutoka Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP), Rodgers Dhliwayo akiwasilisha mada kuhusu namna ya kuyafikia Malengo Mapya 17 ya dunia wakati wa Semina ya Wabunge kuhusu malengo hayo mjini Dodoma.PICHA/Aron Msigwa-MAELEZO.

Na Fatma Salum-MAELEZO, Dodoma.


Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wametakiwa  kusimamia vyema utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo kwa kuhakikisha kuwa Serikali inatekeleza mipango iliyojiwekea kwa wakati ili kuimarisha ustawi wa wananchi wanaowawakilisha na taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Dodoma na Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson  wakati akifungua semina fupi ya Wabunge kuhusu Malengo Endelevu ya Maendeleo ya Dunia iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa kupitia mpango wake wa kufanya kazi pamoja  (Delivery as One).

Dkt. Tulia amesema kuwa Wabunge wana  jukumu la kuzingatia malengo hayo na kuhakikisha yanatekelezwa kwa kuwa mipango yote na mikakati ya maendeleo hupitia Bungeni hivyo hawana budi kusimamia malengo hayo ipasavyo kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.

Akizungumza wakati wa semina hiyo Mwakilishi Mkaazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Bw. Alvaro Rodriguez amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli  inafanya kazi nzuri katika utekelezaji wa Malengo Endelevu ya Maendeleo ya Dunia na kuwataka Wabunge kuwa mabalozi wazuri katika utekelezaji wa malengo hayo.

Bw. Rodriguez ameongeza kuwa ni muhimu sana kwa Wabunge kuweza kuyaelewa malengo hayo ya Dunia ili waweze kufanikisha utekelezaji na ufuatiliaji wake katika ngazi zote za Taifa.

Mwaka 2015 nchi 193 ikiwemo Tanzania zilikubaliana kwa pamoja kutekeleza mkakati wa kumaliza umaskini, kupambana na mabadiliko ya tabia nchi na kupigania haki na usawa. Katika kufanikisha hilo nchi hizo zilikubaliana kupitisha Malengo Endelevu 17 ambayo ni Kutokomeza Umaskini, Kukomesha Njaa, Afya Njema na Ustawi, Elimu Bora, Usawa wa Jinsia, Maji Salama na Usafi, Nishati Mbadala kwa Gharama Nafuu, Kazi zenye Staha na Ukuzaji Uchumi, Viwanda, Ubunifu na Miundombinu, Kupunguza Tofauti.

Malengo mengine yaliyoafikiwa na nchi hizo ni Matumizi na Uzalishaji wenye Uwajibikaji, Miji na Jamii Endelevu, Kuchukua Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabia Nchi, Kuendeleza Uhai katika Maji, Kulinda Uhai katika Ardhi, Amani, Haki na Taasisi Madhubuti na Ushirikiano ili Kufanikisha Malengo.

Naye Naibu Katibu Mtendaji Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Maduka Paul Kessy amesema kuwa Tanzania imejipanga kutekeleza malengo hayo kwa ufanisi ili kufikia azma ya kuiondoa nchi yetu miongoni mwa nchi maskini na kuiwezesha kuwa nchi ya uchumi wa kati na maendeleo ya viwanda.

“Utekelezaji wa malengo haya utakwenda sanjari na utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano ambao msingi wake ni kuchochea mabadiliko ya uchumi na maendeleo ya watu.” Alisema Kessy.
















No comments: