Saturday, May 28, 2016

WANANCHI WAFURIKA BANDA LA BENKI YA NMB KATIKA MAONESHO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI UWANJA WA CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI.

Mgeni Rasmi katika Maonesho ya Wakulima na Wafugaji,Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala manispaa ya Moshi,Wencelaus Lindi akitia saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Benki ya NMB katika maeonesho hayo yanayofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika mjini Moshi.
Meneja Mwandamizi wa Mahusiano ya biashara na Kilimo wa Benki ya NMB,Oscar Rwechungura (aliyenyoosha kidole) akitoa maelezo kwa mgeni rasmi ,Wencelaus Lindi (aliyekunja mikono) katika maonesho ya Wakulima na Wafugaji yaliyoandaliwa na Mtandao wa kusaidia wakulima wa AgriProFocus.
Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi,Emanuel Kashusho akikabidhi zawadi ya T-shirt ,Kalamu na Key holder kwa mgeni rasmi ,Wencelaus Lindi mara baada ya kutembelea banda la Benki hiyo na kupata maelezo namna inavyoshirikiana na wakulima katika kukuza mitaji yao.
Mgeni rasmi ,Wencelaus Lindi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NMB pamoja na wananchi wengine waliofika kutembelea banda la NMB.
Meneja Mwandamizi wa Mahusiano ya biashara na Kilimo wa Benki ya NMB,Oscar Rwechungura akitoa maelezo kwa baadhi ya watu waliotembelea banda hilo.
Afisa Mikoapo wa Benki ya NMB,Gaudencia Mazigo akigawa vipeperushi kwa wananchi waliofika katika banda la Benki hiyo katika maonesho ya wakulima na wafugaji yanaoyofanyika katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Afisa Mikopo wa Benki ya NMB,Josephine Joseph akitoa maelezo kwa wateja waliofika kutembelea banda la NMB wakati wa maoenesho ya Wakulima na Wafugaji yanayofanyika katika uwanja wa chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Afisa Mikoapo wa Benki ya NMB,Gaudencia Mazigo akigawa vipeperushi kwa wananchi waliofika katika banda la Benki hiyo katika maonesho ya wakulima na wafugaji yanaoyofanyika katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika Moshi.  
Meneja Mwandamizi wa Mahusiano ya biashara na Kilimo wa Benki ya NMB,Oscar Rwechungura akitoa maelezo kwa mmoja wa watu waliotembelea banda la NMB.
Meneja wa NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi Emanuel Kashusho akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi waliotembelea banda la NMB wakati wa maoensho ya Wakulima na Wafugaji.
Baadhi ya wananchi wakiwa katika banda la NMB.

Imeandaliwa na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog kanda ya Kaskazini.

No comments: