Wednesday, May 25, 2016

Serikali yaadhimisha siku ya Afrika kwa kumuenzi nguli mpigania uhuru wa Tanganyika Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Halfan Mshiro pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema wakiokota baadhi ya uchafu katika kaburi la nguli mpigania Uhuru wa Tanganyika Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta walipozuru kaburi hilo katika kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni mtoto wa tano wa hayati sheikh Kaluta Bw. Amiri Kaluta Amri Abedi na kulia ni Naibu Meya Bw. Salum Faisal.
Mtoto wa tano wa hayati sheikh Kaluta Bw. Amiri Kaluta Amri Abedi (watatu kulia) akiongoza dua ya kumuombea baba yake hayati sheikh Kaluta Amri Abeid wakati ujembe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli huyo kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema (kushoto mbele) akizungumza wakati ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli mpigania Uhuru wa Tanganyika Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo Bibi. Nuru Halfan Mshiro.
Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa Dkt. Suleimani Sewangi (mwenye miwani) akisoma tawasifu ya hayati Sheikh Kaluta Amri Abeid Kaluta wakati ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli huyo kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa Dkt. Suleimani Sewangi (mwenye miwani) akisoma tawasifu ya hayati Sheikh Kaluta Amri Abeid Kaluta wakati ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli huyo kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
 Bw. Kassim Amotile (mwenye miwani) akigani Shairi lililoandikwa na marehemu Mathias Mnyampala mwaka 1964 wakati wa kifo cha hayati Sheikh Kaluta Amri Abeid Kaluta na kulipa jina la Kifo cha Sheikh Abeid, Pengo kuu kwa Taifa wakati ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipozuru katika kaburi la nguli huyo kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema na wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara hiyo Bibi Nuru Halfan Mrisho.Picha na: Genofeva Matemu - Maelezo
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sofia Mjema (kulia) akiongoza msafara wa ujembe kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuzuru Kaburi la nguli mpigania Uhuru wa Tanganyika Hayati Kaluta Amri Abeid Kaluta katika kuadhimisha siku ya Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo Bibi. Nuru Halfan Mshiro na kushoto ni Naibu Meya Bw. Salum Faisal.

No comments: