Monday, May 2, 2016

MBUNGE WA JIMBO LA VUNJO ATEMBELEA BARABARA YA KILEMA NA KUJIONEA ILIVYO HARIBIKA VIBAYA KUTOKANA NA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA


Mbunge wa Jimbo la Vunjo ,James Mbatia akitizama barabara ya kuelekea Hospitali ya wilaya ,Kilema Hospital namna ambavyo imeharibika kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha.
Wanafunzi katika shule iliyo jirani na barabara hiyo wakitizama sehemu ya korongo lililopo katika barabara hiyo ambayo ni tegemeo kwa Chuo cha Ualimu Mandaka,Seminari ya Mtakatifu James ,shle za sekondari pamoja na msingi.


Baaadhi ya madreva wa pikipiki maarufu kama bodaboda wakipita katika barabara hiyo ambapo kwa sasa nauli ya kupandisha abiria kwenda Hospitali ya wilaya ya Moshi,Kilima imepanda kutoka kiasi cha sh 3000 hadi 6000 .
Moja ya Magari yanayotumia barabara hiyo likijaribu kupita katika barabar hiyo ambayo imeharibika vibaya kutokana na maji yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.
Sehemu ya barabara hiyo likionekana korongo ambalo limeanza kumegwa na maji na kuhatarisha kukatika kwa mawasiliano katika baina ya vijiji 12 ambavyo wakazi wake wanatumia barabara hiyo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: