Wednesday, May 25, 2016

AHADI YA RAIS JPM KUHUSU MAJI MJI WA ILULA KUTEKELEZWA -WAZIRI LWENGE

Bw Venance Mwamoto.

Na MatukiodaimaBlog
WAZIRI  wa maji na  umwagiliaji mhadisi Geryson Lwenge amewaondoa  hofu   wananchi  wa  mji  wa Ilula  wilaya ya  Kilolo  mkoani Iringa kuhusu  ahadi  ya Rais Dr John Magufuli ya  kumaliza kero ya  maji  katika  mji  huo  wa Ilula kuwa  itaanza kutekelezwa mwaka  huu.

Alisema  kuwa serikali  ya  awamu ya  tano  chini ya  Rais Dr Magufuli  ni  serikali ya ukweli na  uwazi na ni  serikali ya  hapa  kazi Tu  hivyo kila ilichoahidi  kukifanya  itafanya kwa  wakati na  kuwataka  wananchi  kuendelea kujenga  imani  zaidi.
  
Waziri mhandisi  Lwenge aliyasema  hayo jana katika Mgahawa wa Bunge mjini  Dodoma , wakati  akizungumza katika  kikao chake na mbunge wa  jimbo la Kilolo Venance Mwamoto na mbunge wa viti maalum mkoa  wa Iringa Ritta Kabati na wawakilishi   11 wa wananchi  wa mji  wa Ilula waliofika bungeni  mjini Dodoma kufuatilia ahadi ya maji  iliyotolewa na Rais Dr  Magufuli  wakati wa kampeni kwa wananchi  wa mji  wa Ilula .  
 Mwamoto  akishiriki na  wananchi wa mji wa Ilula  kukinga maji ambayo hutoka kwa mgao.

Alisema  kuwa wizara  yake  imekwisha  ingiza  katika bajeti  yake ya mwaka 2016/2017 itakayosomwa mapema wiki  hii na  kuwa mbali ya  maeneo  mengine ambayo  yatapatiwa ufumbuzi  wa  kero ya maji mji  wa Ilula ni  miongoni mwa maeneo  hayo .

Waziri  huyo  alisema  kuwa lengo la  serikali ni  kuendelea  kusogeza  huduma ya  maji kwa  wananchi  wake na  kutekeleza ahadi  zake kupitia  ilani ya uchaguzi ya  chama tawala hivyo.

Hata  hivyo  waziri Lwenge  alimpongeza mbunge  wa Kilolo Bw Mwamoto na mbunge Kabati  kwa kuendelea  kupambana  bungeni kwa ajili ya kuwatumikia  wananchi  wao na  hata   kufuatilia baadhi ya ahadi  na  kuwa hatua hiyo ni nzuri na  inaonyesha  ni  kiasi gani wabunge  wao  walivyokaribu na changamoto  za  wananchi  wao.

Mbali ya waziri Lwenge  kuzungumza na  wananchi hao pia  mbunge  Mwamoto  aliwakutanisha  wananchi hao na  waziri  wa Kilimo ,mifugo na Uvuvi  Mwigulu Nchemba ambae katika  kikao  chake na  wananchi hao  alieleza mkakati wa   wizara yake  kushirikiana na  wizara ya viwanda na biashara pamoja na  wizara ya vijana na ajira ili  kuanzisha viwanda  vidogo vya  nyanya katika  mji  wa Ilula na  kuwa kazi ya  wizara  yake ni  kutoa mafunzo ya  kilimo cha  kisasa cha nyanya na  kuwawezesha  wakulima hao  wa mafano mpango ambao   utafanyika katika kanda mbali mbali ila kwa nyanda za juu  kusini  wanakusudia  kuufanya  wilaya ya Kilolo .
Kijana  wa Ilula  akichambua nyanya.

Kwa  upande  wake waziri  wa vijana na ajira Antony Mavunde alisema  kuwa wizara  yake  ipo  tayari  kuwasaidia  vijana katika  wilaya ya  Kilolo kwani  tayari  wameonyesha  nia ya  kujikwamua  kiuchumi  kupitia  kilimo  cha nyanya na  kuwa kazi ambayo  mbunge na  viongozi wa wilaya ya  Kilolo wanapaswa  kuifanya ni kuwaunganisha  vijana  hao katika  vikundi na kuanzisha  Saccos zao  ili  pesa  itakapotolewa na  serikali  kupitia katika  saccos  hiyo .

Alisema  kuwa upo  uwezekano wa vijana hao  kuanzisha  kilimo  cha  nyanya  na  kuwa na  viwanda  vidogo  vya  kuchakata  nyanya na  kuziuza badala ya  sasa  kuuza kwa hasara.

Mbunge  wa Kilolo Bw  Mwamoto aliwapongeza  mawaziri  hao  kwa kuonyesha  utayari  wao katika  kuwasaidia  wananchi  wa Kilolo na  kuwa kilio  kikubwa kwa  wananchi wa mji wa Ilula ni maji ,masoko ya uhakika  ya mazao na hivyo  kusaidiwa maji na vijana  kupata viwanda  vidogo  vidogo  wataweza  kukuza  kilimo cha  kisasa  zaidi.

 Katika ziara  yao  hiyo  bungeni wananchi  hao  ambao ni  wawakilishi  wa  wananchi wa Ilula  waliongozana na katibu  wa chama cha mapinduzi (ccm) wilaya ya  Kilolo Bw Clemence Mponzi na  aliyekuwa diwani wa Ilula Anna Msolla, Peter Mdanginyali , diwani wa kata ya Mlafu Bw  Isdori Kihenge , Vicent Gaifalo,Anna Msolla, kada  wa hadema Bw Khalid  Muhel , Jocob Ngusulu ,Uzebeo Mhando  na katibu tarafa ya Mazombe Bw King’ung’e

No comments: