Saturday, April 16, 2016

WANYAMA PORI WAVAMIA MASHAMBA YA WANANCHI NA KUMALIZA MAZAO YAO

Na Woinde Shizza,Karatu

Wananchi wa kata ya mbulumbulu walalamikia Mmalaka ya hifadhi ya Ngorongoro kushidwa kuzibiti wanyama pori kwani wanaharibu mazao yao.

Hayo waliyasema juzi wakati wa ziara ya mwenyekiti wa CCM mkoa Arusha, Lekule Laizer wakati alipotembelea katika kijiji cah losteti ikiwa ni ziara yake ya kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho.

Walisema kuwa mazao yao yamekuwa yakiaribiwa na wanyama wanaotoka katika hifadhi ya ngorongoro haswa nyakati za jioni na usiku na wametoa taarifa katika uongozi wa mamlaka hiyo lakini hamna hatua zozote ambazo wamezichukuwa.

Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina Aron Saiteu alisema kuwa wanyama hao wamekuwa wanakuja katika mashamba yao ambayo wameotesha mahindi na maharage na kuingia na kula hali ambayo inawarudisha nyuma kimaendeleo na inawakosesha chakula.

Alisema kuwa wamepeleka taarifa za malalamiko katika kituo kidogo ambacho kipo katika eneo hilo lakini hadi sasa hamna kiongozi ambaye amechukuwa hatua .

“awali tulikuwa tunawafukuza wanyama hawa lakini mamlaka ikaja na kutunyima kufukuza wanyama lakini cha kushangaza mara baada ya kutuzuia kufukuza wakatuambia tukiona mnyama tumpige simu tatizo lililokuja ukipiga simu unaambiwa na viongozi ambao wapo apa katika kituo cha wanyama pori cha losteti wanasema awana magari hivyo awawezi kuja kufukuza wanyama sasa na sisi wananchi tunashindwa tufanyaje unakuta tembo kaja au mbogo ivi unamfukuzaje jamani inabidi uache ale akitosheka aondoke “alisema Seuri lazier

Alisema kuwa hali iyo inatokea sana hawa katika kipindi hichi mazao yao yametoka na wananyama hao usogea maeneo hayo kuanzia majira ya saa kumi na mbili jioni na hata saa kumi na mbili asubui unaweza ukawakuta wananyama hao wakiwa mashambani kwa watu.

Aidha aliongeza kuwa kunakituo cha ngongoro kipo karibu na kijiji hicho na pindi wanapopiga simu pale ili wapatiwe ufumbuzi wa kufukuziwa wanyama hawa wamekuwa wakijibiwa kuwa ofisi hiyo haina gari na badala yake wanawaambia wananchi wapige simu makao makuu ya hifadhi kuomba gari litakalo saidia doria ya ulinzi wa mashamba juu ya wanayama pori .

Aidha walifafanua kuwa kwakuwa tatizo hili limekuwa linatokea mara kwamara wanaomba basi serekali au mamlaka husiku kusaidia kulipa angalau fidia ya nusu ya mazao ambayo yameliwa na wanyama hawa ili angalau mwananchi asipate hasara ya moja kwa moja .

Akiongelea swala hilo mkuu wa idara ya uhifadhi ambaye pia ni kaimu muhifadhi mkuu wa hifadhi hiyo Izrael Namani alisema kuwa swala hilo sio la kweli kwani kwanza kabisa mamlaka ina ofisi pembezoni mwa kijiji hicho kinacholalamikiwa huku akisema kuwa pia mamlaka ina gari ya kufanya doria za mara kwa mara katika mipaka yote ya hifadhi .

Alisema kuwa pia swal ahili lipo chini ya idara ya wanyama pori lakini wao kama hifadhi ya ngorongoro kupitia idara ya ujirani mwema wamekuwa wakishirikiana kw aukaribu na wananchi katika kufanikisha mambo mengi ikiwemo ya wanyama kutoharibu mazao.

Aliongeza kuwa pamoja kuna changamoto mbalimbali lakini pia wanajitaidi kwa hali namali kuhakikisha wanayama wanakaa katika maeneo yao na kutoleta mathara kwa wananchi na mali zao.

“unajua kwa mipaka ya hifadhi ni mingi na sio mda wote unaweza kuta askari yupo katika kila eneo lakini pindi tunapopata taarifa tunatuma askari wetu wawanyama pori na waenda kwa muda unaotakiw akutatua tatizo hilo mfano ata awa wananchi wakipiga simu kiukweli apa nata nizungumzie swal ala gari ndugu mwandishi umeona geografia ya hayo maeneo kuna sehemu ambayo gari aiwezi fika sasa apo kweli unafanya inabidi ufike gari inapofika alafu uanze kutembea na miguu lakini swala ambalo wanasema atuwapi ushirikiano sio kweli’alisema Namani.

Aidha alisema kuwa kwa upande wa swal ala fidia wao kama mamlaka ya ngorongoro hawana fidia yeyote wanao toa ila kuna mkono wa pole ambao unatolewa kwa muadhirika kutoka kwa mamlaka ya idara ya wanyama pori na hiii sio fedha iliopangwa ni kiasi Fulani bali ni chochote kile kitakachopatikana.

Gazeti hili lilimtafuta pia Afisa maliasili wa wilaya ya katatu Staley Mruma ambaye yeye pia ni mlengwa mkuu anaesimamia wanyama pindi pale wanapotoka nje ya hifadhi naye alisema kuwa wao kama idara ya maliasili kwa kushirikiana na mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro wamekaa kikao march 19 cha kuangalia jinsi ya kukabiliana na tatizo hili na walikubaliana kushirikiana kutatua tatizo hili na kufuta kauli ya kusema wanyama ni wa mamalaka fulani bali waliamua kwa pamoja kwa kusema wanyama ni wawatu wote.

Alibainisha kuwa kwa sasa ivi wameweka mikakati wa kufanya doria kwa pamoja wao pamoja na hifadhi ya ngorongoro ,pia waliagiza magari yaongezwe ili yafikie nane ambayo yataweza kufikia katika kila mpaka ,huku akibanisha kuwa katika kikao hicho pia walipanga kufanya vikao vinne kila mwaka kwa ajili ya kujadili changamoto zilizopo katika mipaka ya hifadhi hiyo.

Aidha alisema kuwa kwa upande wa malipo au fidia ambazo wanalalamikia wananchi wao kama idara ya maliasili wanamfuko wa kutoa pole na mpaka sasa unafanya kazi kwani kipindi cha mwaka jana mwezi wasita waliwalipa kifuta jasho wananchi ambao wamearibiwa mazao yao ambapo alisema jumla ya wananchi 52 walilipwa kifuta jasho hicho.

"kuna wananchi ambao tumeshawalipa kifutajasho kutokana na kuaribiwa mazao yao na wanyama lakini sio wote kunabaadhi ambao bado awajalipa walishaleta malalamiko yao na sisi tukayapeleka wizarani kwa iyo tunasubiri majibu yakija tu hivi tutawalipa kifutajasho chao"alisema mruma.

Aidha aliongeza kuwa katika watu hao wanaodai kifutajasho chao kuna wananchi sita ambao hawajalipwa kwani wao walifariki mara baada ya kuzuriwa na wananyama tofauti tofauti kwa nayakati tofauti lakini sio kwamba hawata lipwa na swala lao lilishapelekwa wizarani na wanasubiri kifuta jasho chao kije na kikifika watalipwa ndugu zao.

Alibaini vijiji ambavyo vilikuwa vinadai fidia na baadhi yao vimeshalipwa kuwa ni pamoja na kambi ya simba ,kitete,lostate pamoja na slahamu huku akisema kuwa wananchi wasiwe na wasiwasi kwani wao kama maliasili kwa kushirikiana na hifadhi ya ngorongoro wanaakikisha kunakuwa na ulinzi wa kutosha.

No comments: