Thursday, April 7, 2016

UMOJA WA ULAYA(EU) WAZINDUA PROGRAMU WA KUZISAIDIA ASASI ZISIZO ZA KISERIKALI HAPA NCHINI.

Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Bw. Roeland Van De Geer kizungumza jambo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa programu ya kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali iliyofanyika jana. Picha na Geofrey Adroph
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya(EU) kutoka Brussels, Bi Rosario Bento Pais akizungumzia masuala ya kuzisaidia asasi zisizo za kiserikali ili ziweze kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa maana hizo zinawalenga watu katika jamii husika.
Mwakilishi wa asasi za kiraia, Bw. Francis Kiwanga akizungumza juu ya ushirikiano wa Umoja wa Ulaya(EU) ulivyoamua kuzisaidia asasi zisizo za kiserikali za Tanzania Bara pamoja na Zanzibar. Maeneo ambayo Umoja wa Ulaya inajikita nayo katika asasi zisizo za kiserikari ni tatu amabazo ni kuweka mazingira bora kwa mashirika yasiyo ya kiserikali kufanya kazi katika mazingira bora hapa nchini, pili ni kuyajengea uwezo mashirika hayo na mwisho nikufanya kazi katika Sere pamoja na sheria ili kuwa na sheria bora na nzuri kwa maendelea ya nchi yetu.
Baadhi ya mabalozi kutoka Umoja wa Ulaya(EU) pamoja na wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa programu ya kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali iliyofanyika jana
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya(EU) kutoka Brussels, Bi Rosario Bento Pais(kulia) akisaini kuashiria uzinduzi rasmi wa programu ya kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali kushoto ni Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania,Bw. Roeland Van De Geer
Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania,Bw. Roeland Van De Geer(kushoto) pamoja na Mwakilishi wa asasi za kiraia, Bw. Francis Kiwanga wakisaini kuashiria uzinduzi rasmi wa programu ya kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali za Tanzania Bara na Zanzibar. Katikati ni Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya(EU) kutoka Brussels, Bi Rosario Bento Pais
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya(EU) kutoka Brussels, Bi Rosario Bento Pais(kushoto), Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania,Bw. Roeland Van De Geer(katikati) pamoja na Mwakilishi wa asasi za kiraia, Bw. Francis Kiwanga wakizindua rasmi programu ya kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali za Tanzania Bara na Zanzibar.
Picha ya Pamoja.

No comments: